Baba Mtakatifu Francisko amekutana na Makardinali katika Mkutano mdogo Vatican
na kuruhusu kutangazwa watakatifu watoto wawili wa Fatima kuwa watakatifu tarehe 13
Mei 2017 ambao ni Mwenye heri Francisko Marto, aliyezaliwa 11 Juni 1908 na kifo
chake kikatokea hapo 4 Aprili 1919 na Mwenyeheri Yacinta Marto, aliyezaliwa 11 Machi
1910 na kifo chake 20 Februari 1920, hawa watoto ni ndugu wawili wa Fatima.
Wengine watatangazwa watakatifu tarehe 15 Oktoba 2017 ambao ni Angelo da Acri Padri
wa Shirika la ndugu wadogo Wakapuchini aliyezaliwa Oktoba 1669 na kifo chake 30 Oktoba
1739. Faustino Míguez, padre wa Shirika la Scolopi na mwanzilishi wa Shirika la Calasanziano
wa watawa wa kike Mchungaji mwema;
Mwenye heri Andrea de Soveral na Ambrogio Francesco Ferro,mapadre wa Jimbo na Matteo
Moreira, mlei na wanzake 27 mashahidi waliouwawa kwa ajili ya kutetea imani yao nchini
Brazil tarehe 16 Julai 1645 na tarehe 3 Oktoba 1645. Na mwisho Cristoforo, Antonio
na Giovanni, vijana mashahidi walio uwawa kwa ajili ya kutetea imani yao nchini Mexco
mwaka 1529.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.
All the contents on this site are copyrighted ©. |