Tumekuwa na misukosuko kwa wiki tatu nchini Afrika ya Kusini na kuna wasiwasi mwingi
kuhusu hali ya baadaye na siyo tu kuhusu wasiwasi wa kiuchumi. Mara nyingi kinacho
tokea Afrika Kusini huathiri vibaya hata nchi ya Botswana na Swaziland. Hali ya kutokuwa
na uhakika pia ukosefu wa kuaminiana,huo ni uzoefu karibu unao ikumbuka dunia nzima,
kwa namna hiyo hata kama faraja ni ndogo,sisi hatuko peke yetu kwa jambo hili.
Huu ni ujumbe wa Pasaka kwa mwaka 2017 wa Baraza la Maaskofu wa Afrika ya kusini
unao wapa matumaini waamini wake wote kwa kipindi hiki chenye msukosuko ya nchi,Maaskofu
wamesema, ni vigumu kuishi bila kuwa na uhakika kwa maana hali hiyo uongeza wasiwasi
ambao unaweza kugeuka na kuathiri vibaya uhusiano kwa watu wengine.
Kwa njia hiyo ujumbe wa Pasaka unaeleza kwamba, waamini watambue kuwa hawapo peke yao kwa sababu Kristo yuko pamoja nao. Yeye kamwe hawaachi watu wake, anatembea nao wakati wote kuhimarisha na kufariji.Kwa njia hiyo Maaskofu wamesema, kamwe watu wasikate tamaa .Pasaka ni sherehe inayo kumbusha kwamba "sisi ni Pasaka ya watu, yaani watu wenye kuwa na matumaini na walio jazwa na maisha ya Roho Mtakatifu wa Mungu.Ni katika furaha na katika matatizo yetu, na katika matatizo yetu ndimo Bwana amefufuka ; Kristo ni mshindi , Kristo ni Mfalme pia Kristo ni mtawala”! (Christus vincit! Christus regnat! Christus imperat!).Ushindi wake tumepewa sisi ili tuweza kuutoa kwa watu wangine, ule mwanga wa matumaini na furaha ambayo uangaza katika giza na vivuli!.
Ujumbe ulio sahini wa na Rais wa Baraza la Maskofu wa Afrika ya Kusini ,Askofu Mkuu Stephen Brislin, unasema ,kwa niaba ya Baraza la Maaskofu wa Afrika ya Kusini ,wanawatakia Baraka na Heri ya Pasaka Takatifu watu wote wa Botswana,Afrika ya Kusini na Swaziland. Mungu abariki familia zao na kuwapa neema ili uwepo umoja na maelewano katika familia zao. Wawe na furaha na utulivu kwa wakati huu ambao ni uthibitisho wa matumaini.Ujumbe unahitimisha na maneno ya kufariji kupitia maneno ya Nabii Isaya yasemayo “Basi,usiogope, mimi nipo pamoja nawe.Usifadhaike, mimi ni Mungu wako.Nitakuimarisha na kukusaidia;nitakulinda kwa mkono wangu wa ushindi”. (Isaya 41:10)
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |