Askofu George Desmond Tambala wa Jimbo la Zomba na Rais wa umoja wa watawa wa kike
na kiume nchini Malawi, amewataka watawa kujikita katika mabadiliko ya Jamii , kiuchumi
na kisiasa kwamba ni kuingia katika uzoefu wa ulimwengu ikiwemo nchi ya Malawi.
Askofu Tambala aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Mkutano mkuu wa 57 wa mwaka wa
Umoja wa watawa Katoliki nchini Malawi, ambapo siku nne za mkutano huo zilifanyikia
mjini Lilongwe. Askofu anasema kwasasa jamii ya Malawi inaendelea kubadilika kwa kina
ambapo watawa wa kike na kiume hawana budi kwa makini kupokea mabadiliko hayo.
Jamii inabadilika, na hasa kuona namna ya kumfikiria Mungu, na maadili, ni mabadiliko
ya kutokumjua Mungu katika maisha ya raia, kwenye mtazamo wa kumuondolea mtu haki
zake, uhuru wake, hadi kufikia kupoteza maana ya historia na maendeleo endelevu ya
mtu.Anasema Askofu Tambala.Askofu huyo ambaye pia ni mtawa wa Shirika la Wakarmeli,
anasema,sera za kisiasa kwa upande wa wanasisa na vyama pia vina changia suala hili,badala
ya siasa kujikita katika kueneza na kuendeleza mabadiliko chanya ya jamii.
Naye Katibu Mkuu wa Umoja wa watawa Sr Mary Madalen Ndawala, anasema katika Mkutano
wenye kauli mbiu “ kuingia kwa mabadiliko ya Ulimwengu ndani ya maisha ya kitawa”,
umekuwa ni muhimu sana kwa kuudhuliwa na wakuu wa mashirika 28 kutoka katika mashirika
mbalimbali ya wanawake wanao hudumia Bwana katika majimbo mbalimbali nchini Malawi.
Na kwamba lengo kubwa ni kuwahimarisha watawa kwa kile ambacho tayari ulimwengu umepokea,
kwani wakuu wa mashirika ni viongozi ambao wanapaswa kujua mabadiliko ya ulimwengu
wa sasa na kwa njia hiyo waweze kufanya uzoefu kama viongozi wa mashirika yao.Hali
kadhalika kama kiongzoi ndani ya Jumuiya anapaswa kuwa mtaalamu wa uchumi, jamii na
mabadiliko ya kisiasa yanayotokea na kwa njia hiyo anahitaji kubadilsiaha uzoefu
wake na wengine kwa kile ambacho amekipokea kutoka katika mkutano huu na hivyo anasema
,tunatarajia viongozi wa mashirika walio udhuria mkutano huo wapate kuwashirikisha
watawa wenzao mara warudipo katika jumuiya zao.
Aidha anasema kwa upande wa mabadiliko ya uchumi , tunataka hawali ya yote iwe chemichemi
katika uendeshaji na kujitegemea,pia katika mabadiliko ya kijamii, ni lazima kukumbatia
aina mpya za kiteknolojia , lakini kuifanya kwa uangalifu na uwajibika kama njia mojawapo
ya kwanza ya uinjilishaji katika jamii.Sr Ndawala pia anasema pamoja na kwamba sisi
siyo wasaidizi lakini pia ni jukumu letu kushauri wanasiasa inapobidi ushiriki wetu
katika siasa.Kati ya waliondesha mkutano wa mwaka ni pamojana na Padre Andrew Kaufa,
kutoka katika Shirika la wamisionari wa Montfort (SMM) na Mkurugenzi wa Televisheni
ya Luntha Padre Emmanuel Chikaya wa Shirika la Kitawa la Wakarmeli
Na (Prince Henderson in Malawi)
All the contents on this site are copyrighted ©. |