2017-02-14 15:25:00

AMECEA kujikita katika kulinda watoto na wenye mazingira magumu


Katika jitihada za kuendelea kulea na kulinda watoto,Idara ya kichungaji ya  AMECEA imeandaa semina mbayo inalenga jinsi gani mkutano ya Baraza la Maaskofu Kitaifa na majimbo wamekabiliana namna gani kujibu sula hli kwa miaka hii.
Ni wiki mbili za semina iliyo anza huko Malindi nchi Kenya kuanzia tarehe 12 hadi 25 Februari 2017. Semina hiyo ina washiriki 40 kutoka miongoni mwa nchi tano za AMECEA ambao ni wajumbe kutoka  Ethiopia,Kenya,Malawi, Sudani ya Kusini na Zimbabwe.Mkutano huo pia unaudhuliwa na Sr Kayula Lesa mjumbe wa tume kwa ajili ya ulinzi wa watoto Vatican, Askofu wa Jimbo la Malindi Emanuel Barbara, Askofu wa Jimbo la Nakuru Maurice Muhatia na katibu Mkuu wa Amecea Padri Ferdinand Lugonza.


Katika lengo kuu la kuanzisha muongozo wa  kina juu ya sera za ulinzi wa watoto ni kwamba kila Baraza la maaskofu wa kila Jimbo watatakiwa kuchota taratibu na kanuni za pamoja ambazo zitawawezesha kusaidia kulea, kuheshimu na kulinda watoto katika malezi yao.Aidha mpango huo pia una lengo la kujenga mazingira mazuri kwa ajili ya watu na kutafuta njia mbalimbali za kulinda watoto na watu wanao ishi katika mazingira mangumu.Kwa njia hiyo hatimaye itawezesha Sekretarieti ya AMECEA kukusanya kutoka katika mikutano ya Baraza juu ya  maadili sahii  ya ulinzi wa watoto  kutokana na kile ambacho watakuwa wamejifunza na kuchora ramani kamili ya sera zao watakazokuwa wamekubaliana.

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.