TANZIA: Askofu mstaafu Raymond Mwanyika wa jimbo Katoliki Njombe afariki dunia
Askofu mstaafu Raymond Mwanyika wa Jimbo Katoliki Njombe, amefariki dunia tarehe 24
Oktoba 2013, akiwa na umri wa miaka 83. Alizaliwa kunako mwaka 1930. Baada ya masomo
na majiundo yake ya kikasisi, akapadrishwa kunako tarehe 11 Oktoba 1959.
Baba
Mtakatifu Paulo wa sita, akamteua kuwa Askofu tarehe 16 Januari 1971 na hatimaye kuwekwa
wakfu hapo tarehe 25 Aprili 1971. Baada ya kuwatumikia Watu wa Mungu, Jimbo Katoliki
la Njombe kwa moyo na akili zake zote, akang'atuka kutoka madarakani hapo tarehe 8
Juni 2002.
Marehemu Askofu Raymond Mwanyika atakumbukwa na wengi kutokana
na mchango wake mkubwa wa maendeleo endelevu kwa wananchi wa Njombe. Anatarajiwa kuzikwa
hapo tarehe 29 Oktoba 2013.