2018-06-04 13:59:00

Baba Mtakatifu Francisko akutana na Rais wa Baviera Bw. Markus Soder


Tarehe 1 Juni 2018, Saa 4.30 za asubuhi, Baba Mtakatifu Francisko  alikutana na Rais  Markus Söder wa nchi huru ya Baviera na wajumbe wake alioambatana nao mjini Vatican. Baada ya mazungumzo na utamaduni wa kubadilishana zawadi, Rais  Soder amekwenda katika Monasteri ya Mater Ecclesiae ili kumsalimia Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto XVI.

Aidha taarifa zinasema kuwa, mapema wiki hii, imezinduliwa kwa afla  Picha ya Bikira Maria wa Rosari wa Guatemala kwa ushriki wa viongozi wa Vatican, wa Kanisa la Guatelana na viongozi wa Kidiplomasia waliopo Vatican, katika Bustani za Vatican. Mwenyekiti wa Utawala wa Serikali ya Mji wa Vatican Kardinali  Guseppe Bertello, ndiye aliye  adhimisha ufunguzi huo katika Bustani za Vatican ambapo pia ametoa  shukrani kwa Rais wa nchi ya Guatemala  na baadaye kubariki picha ya Bikira Maria baada ya kuifunua na kuizindua rasmi katika bustani za Vatican.

Picha ya Bikira Maria wa Rosari, ambaye ni msimamizi wa nchi ya Guatemala, inaingia kufanya historia ya kumbukumbu ya miaka 50 tangu madhabahu ya Mama Yetu wa Rosari, kutabarukiwa katika nchi ya  Guatemala barani Amerika ya Kusini kwa utashi wa Mwenyeheri Papa Paulo VI.

 Sr Angela Rwezaula 
Vatican News








All the contents on this site are copyrighted ©.