Siku ya leo ni Sikukuu ya Pentekoste ambayo inahitimisha kipindi cha Pasaka, kipindi
kilichokuwa kinajikitia kutafakari juu ya Kifo na ufufuko wa Yesu. Sikukuu hii inakumbisha
na kuishi uvuvio wa Roho Mtakatifu juu ya Mitume na wengine walio kuwa wameunganika
katika sala na Bikira Maria katika Ukumbi Mkuu (taz Mdo 2,1-11). Siku hiyo ndiyo ilianza
historia ya Takatifu kikristo kwasababu Roho Mtakatifu ambaye ndiye kisima cha utakatifu
na ambaye si kwa ajili ya wachache tu bali ni wito kwa wote.
Ni utangulizi wa Tafakari ya Baba Mtakatifu Francisko, Jumapili 20 Mei 2018 wakati
wa kusali sala ya malkia wa Mbingu, mama Kanisa akiadhimisha Sikukuu ya Pentekoste.
Katika tafakari yake kwa mahujaji na waamini wote walio kusanyika katika Kiwanja cha
Mtakatifu Petro, Baba Mtakatifu amesema, katika ubatizo kwa hakika wote tunaalikwa
kushiriki maisha yenyewe ya Mungu katika Kristo, katika Kipaimara tunageuka kuwa mashuhuda
wake katika dunia. Roho Mtakatifu ananyunyizia utakatifu kila mahali kwa watu waamini
watakatifu wa Mungu (Wosia wa Gaudete et exsultate, 6).
Kama Mtaguso wa Pili wa Vatican usemavyo, Mungu anapenda kutakatifuza watu wote kwa
kila nafsi na kufanya mahusiano kati yao na kuwaunganisha watu hao kwa mujibu wa
ukweli na kuhudumia katika utakatifu (taza Lumen gentium, 9). Baba Mtakatifu amesema,
hata hivyo katika Agano la kale manabii wa Bwna walikuwa wametoa unabii: “Nami
nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika
hukumu zangu, na kuzitenda. Nanyi mtakaa katika nchi ile niliyowapa baba zenu, nanyi
mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu” (Ez 36,27-28). Pia “kila
atajaye jina la Bwana ataokoka” (Joeli 3,1-2.5). Unabii wote huo unatimilizwa
kwa njia ya Yesu Kristo ambaye ni daraja na uhakika kwa vuvio wa Roho.
Tangu wakati wa Pentekoste hadi nyakati za mwisho utakatifu na ukamilifu ni Kristo ambaye anajionesha kwa wote ambao wanajifungulia matendo hai ya Roho Mtakatifu na kujibisha kuwa wakarimu. Mantiki msingi ya utakatifu ni ile ya kuwa tunda la takatifu la Roho. Roho Mtakatifu anapoingia ndani ya maisha, anashinda ukavu na kufungulia mioyo matumaini na kuweka chachu, hasa katika kukuza ukomavu wa ndani na mahusiano na Mungu na jirani!
Kwa mujibu wa Mtakatifu Paulo anaonesha matunda ya roho Mtakatifu kuwa ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, (Gal 5,22). Kwa njia hiyo tuombe Mama Bikira Maria tuweze kupokea zawadi hizo na hata upyaisho wa Kanisa kwa njia ya Pentekoste ili kulijalia zawadi ya furaha ya kuishi na kushuhudia Injili n, kuitangaza kwa shauku ya kuwa watakatifu kwa njia ya utukufu wa Mungu (Gaudete et exsultate, 177).
Na Sr Angela Rwezaula
Vatican News
All the contents on this site are copyrighted ©. |