Kama kawaida ya nia za maombi ya kila mwezi kupitia mtandao wa kijamii, Baba Mtakatifu Francisko kwa mwezi wa Tano, maombi yake yamewaendea waamini walei wote ambao wako mstari wa mbele kujikita katika maisha ya Kanisa. Baba Mtakatifu Francisko anasema, Kanisa linahitaji ushuhuda wao kuonesha ukweli wa Injili na mifano yao hai ili kuelezea imani kwa njia ya matendo hai na mshikamano! Anawashukuru waamini walei wote ambao kwa moyo wote wako tayari kujihatarisha na hawaogopi, kutoa maisha yao kwa maskini, walio baguliwa na kuwekwa pembezoni ili waweze kuwa na matumaini zaidi ya maisha yao.
Aidha anakazia zaidi wito wa kusali mwezi huu, ili waamini walei waweze kutimiza utume wao maalumu, walio upokea katika ubatizo na kujiweka tayari katika ubunifu wa huduma ndani ya changamoto za ulimwengu wa sasa!
Sr Angela Rwezaula
Vatican News!
All the contents on this site are copyrighted ©. |