Mkuu wa shirika la Don Bosco, Padre Angel Fernandes Artime amefanya ziara yake mji wa kale, Damasko kwa ajili ya kuwatia moyo, furaha na matumaini watu walio jeruhiwa zaidi ya miaka 7 ya vita. Gazeti la Wasalesian wanaandika kuwa, Mkuu wa shirika hilo alifika tangu tarehe 5 Aprili 2018 nchini humo akiwa amesindikizwa na baadhi ya vijana wa Mtakatifu Bosco ambapo waliweza kutembea na roho ya hija kupitia katika barabara aliyopitia Mtume Paulo Mtume wa watu na kuingia katika Kanisa la Mtakatifu Anania.
Katika Kanisa hilo, walisikiliza historia juu ya safari ya uongofu wa Mtakatifu Paulo na mwisho Padre Artime alitoa kutafakari ndogo kuhusu umuhimu wa ushuhuda huo, na jinsi gani unavyotakiwa hata leo hii kwa wote, ili kuweza kubadili mtazamo wa maisha na kuyaelekeza kwa Mungu. Siku ilimazikia katika eneo la Tabbala huko huko Damasco.
Tarehe 6 Aprili Padre Angel Fernandes, aliungana na wanajumuiya wanaoishi na kujikitia kutoa huduma katika maeneo hayo ili kusikiliza matatizo na changamoto wanazokabiliana nazo, pia yeye kuwaonesha ukaribu wake. Mchana aliweza kukutana na watoto, vijana wanaohudumiwa na shirika lake katika eneo hilo, ambapo ni karibia vijana na watoto 1,000. Vijana hao waliweza kutumbuiza nyimbo za burudani na ngoma kumkaribisha mkuu wa shirika hilo na hata yeye katika kushiriki furaha hiyo aliweza kushika gita ana kuimba nao!
Sr Angela Rwezaula
Vatican News!
All the contents on this site are copyrighted ©. |