Ofisi ya habari Vatican inatoa maelezo kuhusu habari uliyotangazwa katika Gazeti la Repubblica nchini Italia juu ya Papa Francisko alipokutana hivi karibuni na Mkurugenzi wa gazeti hilo kwamba, habari hiyo siyo ya kuaminika kwa mujibu wa maneno ya Papa kama ilivyotolewa katika Gazeti hilo.
Na kwa mujibu wa Habari kamili Vatican zinathibitisha kuwa, Papa Francisko alikutana hivi karibuni na mwanzilishi wa Gazeti la kila siku la Repubblica Bwana Scalfari katika mkutano wa faragha ikiwa ni fursa ya kupeana matashi mema ya Pasaka, lakini hawakufanya au kuacha aina yoyote ya mahojiano!
Kwa mujibu wa maelezo hayo pia Ofisi ya habari Vatican, inathibitisha kwamba, kile ambacho kimeandikwa katika gazeti hilo,kifikiriwe kama ni tunda la utunzi wa habari binafsi,ambao lakini ahusiki katika maneno yaliyozungumzwa na Baba Mtakatifu !
Sr Angela Rwezaula
Vatican News!
All the contents on this site are copyrighted ©. |