Papa Francisko anayo nia ya kutembelea Baraza la Makanisa Ulimwenguni katika makao makuu yaliyoko huko Geneva kutokana na tukio la kuadhimisha miaka 70 tangu kuanzishwa kwake. Ziara yake inatarajiwa kufanyika tarehe 21 Juni 2018. Hayo ni maelezo ya kwa mujibu wa Msemaji mkuu wa Vatican Dr. Greg Burke kwa waandishi wa habari, tarehe 2 Machi 2018 akifafanua pia kwamba, mpango nzima wa Ziara yake ya kitume utatangazwa baadaye.
Vile vile tarehe 2 Machi 2018 katika chumba cha mikutano ya habari Vatican wamewakilisha kwa vyombo vya habari mipango yote inayohusu maadhimisho ya miaka 70 ya Baraza la Makanisa Ulimwenguni. Kutokana na ziara hiyo Papa Francisko atakuwa Papa wa tatu kutembelea makao Makuu ya Baraza la kiekumene la Makanisa Ulimwenguni. Mtakatifu Yohane Paulo II alitembelea tarehe 12 Juni 1984, akiwa katika ziara yake ya kichungaji katika Shirikisho la Makanisa ya huko Ulaya Kaskazini. Lakini kabla ya matembezi hayo alitangulia hata Mwenye heri Papa Paulo VI tarehe 19 Juni 1969 miaka 4 baada ya kufunga Mtakaguso wa II wa Vatican.
Sr Angela Rwezaula
Vatican News!
All the contents on this site are copyrighted ©. |