Padre Henry Saindi, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki nchini Malawi anasikitika kutangaza kifo cha Askofu Emmanuel Kanyama wa Jimbo la Dedza, kilichotoke tarehe 17 Februari 2018 nyumbani kwake Kapiri.
Jimbo la Dedza ni jimbo Katoliki nchini Malawi kikipakana na Jimbo Kuu la Lilongwe. Mwaka 2006 jimbo hilo lilikiwa na idadi ya wabatizwa 459.398 kati ya wakazi 1.173.000 wa jimbo hilo, wakiongozwa na hayati Askofu Emmanuel Kanyama.
Mpango na taratibu zote za maadhimisho ya misa na kuaga zitatolewa. Raha ya Milele umpe ee Bwana Askofu Emmanuel Kanyama apumzike kwa Amani. Amina.
Na Sr Angela Rwezaula
Vatican News
All the contents on this site are copyrighted ©. |