2017-12-29 14:22:00

Pamoja daima ni mada ya familia mwaka 2018, katika Kanisa la Ujerumani!


“Pamoja daima, katika safari ya sakaramenti ya ndoa” ni kauli mbiu ambayo imechaguliwa na itakayoongoza katika majimbo na katika maparokia ya ujerumani wakati wa kuadhimisha  sikukuu ya familia tarehe 31 Desemba 2017, na ambayo itasikindiza Kanisa la Ujerumani kwa mwaka mzima wa 2018.
Na kwa maana hiyo kitabu kidogo  cha ufafanuzi zaidi kimetolewa katika kutoa jibu la maombi ya Baba Mtakatifu Francisko kuhusu  kuutafakari na kuunyambulisha  Waraka wake wa Amoris Laetitia, (Furaha ya upendo) ili kuhusisha na kujumuisha kwa kiasi kikubwa jumuiya ya kikristo katika kuwasindikiza familia katika ndoa.

Kitabu kidogo hicho kimegawanyika katika sehemu nne  ambazo zinawakilisha baadhi ya tafakari muhimu ya uzoefu  ambao tayari upo ndani ya familia na kusaidia kutoa neno muhimu  la kuweza kutambua nini maana ya ndoa ya kikristo. Aidha katika kitabu kidogo hicho kimeandikwa hata sala  na maandhimisho mbali yenye mada ya ndoa vilevile wameweka  mkusanyiko wa viunganishi vya vitabu vikubwa  mbalimbali vyenye  marejea ya kupata ufahamu zaidi vilivyopo nchini Ujerumani. 

Mwenyekiti wa Tume ya Baraza la Maaskofu wa Ujerumani,  kwa ajili ya ndoa na familia, Askofu Mkuu Heiner Koch wa Jimbo Kuu la Berlin, katika utangulizi wa kitabu hicho kidogo ametoa ufafanuzi kuwa, majadala mkali uliotokea mwaka huu 2017,  kuhusiana na ufunguzi wa ndoa ya kiraia wa jinsia moja, umeonesha kuwa dhana ya sakramenti ya ndoa bado haitambuliwi kwa walio wengi, kwa maana  hiyo wameamua kuweka nyenzo kama hiyo, ili kuanzia katika maparokia, waamini wanaweza kujadiliana na kukabiliana na mada hiyo muhimu hambayo haiwezi tena kukosa mwelekeo na kuzingatia umuhimu wake kama ilivyokuwa mwanzo.

Askofu Mkuu Koch anafafanua tena kwamba; moja ya matatizo, ni kudumisha uimara wa uhusiano  kati ya mafundisho ya Kanisa juu ya ndoa na michakato yake. Ni siku nyingi sasa wamependekeza kufanya maandalizi ya ndoa katika majimbo na majimbo makuu wakiwa na  madhumuni ya kukabiliana na changamoto za jamii inayobadilika na zaidi, hasa kuwa na wasiwasi wa kukutana na watu katika hali zao za maisha.

Sr Angela Rwezaula
Vatican News

 








All the contents on this site are copyrighted ©.