Mazungumzo na urafiki kindugu kati ya wakatoliki na waorthodox ndiyo misingi ya matunda ya mkutano uliofanyika miaka 50 iliyopita kati ya Patriaki wa Kiekumene Athenagoras na Chiara Lubich. Ndiyo maelezo yaliyomo katika Telegram ya Baba Mtakatifu Francisko aliyotuma katika Taasisi ya Chuo Kikuu cha Sophia cha Wafokolari huko Loppiano Firenze, Italia, kwa Kardinali Giuseppe Bettori, Askofu Mkuu wa Firenze, wakati wa tukio la uzinduzi wa Mkutano wa kimataifa wa Kiekumene wenye kuwa na nia ya kuwaenzi Patriaki wa Kiorthodox na Mwanzilishi wa Wafokolari. Anawapongeza juu ya kufanya kumbukumbu hiyo ya mkutano na kuwatakia matashi mema ili kwamba Chuo Kikuu cha Sophia kwa kufuata karama ya ufunguzi wa Roho, wanaweza kuendelea kuwa sehemu ya makutano na mazungumzo kati ya tamaduni na dini tofauti.
Wazo la mkutano wa Kiekumene katika Chuo Kikuu cha Sofia cha Wafokolari lilianzishwa
tarehe 26 Oktoba 2015, likiwa ni kwa mara ya kwanza, Chuo hicho kinapokea tuzo ya
kwanza ya Shahada kwa ajili ya Utamaduni wa muungano wa Kipatriaki wa kiekuemene wa
Costantinople Bartholomew.
Naye Mwenyekiti wa Wafokolari, Maria Voce, amesema, mpango wa Taaluma hiyo unawakilisha
kipindi muhimu cha mahusiano ya kiekumene ambayo yapo kati ya Makanisa dada wa Mashariki
na Magharibi na kufungua matarajio ya mshangao katika utafiti unaojikitia kuheshimu
mazungumzo, ambayo bado yanahitaji kuwa zawadi ya pamoja katika ngazi ya tafakari
kitaalimungu na muungano wa maandili ya binadamu.
Halikadhalika naye Patriaki Bartholomew ametuma ujumbe wake akionesha furaha yake ya kuanzishwa tukio hilo lenye mada ya “Patriaki wa Athenagora na Chiara Lubich:viongozi wa umoja”. Anaongeza kusema kuwa ni mkutano wa kinabii kati ya mashujaa wakubwa leo hii katika njia ya kiekumene.Anathibisha pia kwamba, mahusiano ya urafiki na ushirikano na Patriaki wa kiekuemene ulianza Juni 1967 ambapo Chiara alikutana na Athenagoras kwa mara ya kwanza. Wakati wa Mkutano wa kwanza alisema, ni jambo zuri kukutana na kutambuana na kwamba, wameishi hivi kiupweke bila kuwa ndugu, bila dada kwa miaka mingi na kama yatima. Karne kumi za kwanza za ukristo zimekuwa ni mafundisho ya Kanisa na kwa ajili ya maandalizi ya Kanisa.Na karne kumi zilizofuta zikawa za kutengana na mivutano, lakini karne ya tatu ni ya upendo.
Katika ujumbe pia Patriaki Bartholomew anasisitiza kuwa, haikuwa tukio la bahati mbaya tendo la Chiara na Athenagora kukutana,bali ilikuwa ni neema ya Mungu ambaye aliweka muhuri kati ya Patriaki wao wa kiekumene na Shirika la Kitume la Wafokolari katika muungano wa upendo kikristo, urafiki wa dhati na mshikamano kindugu ambao unaendelea hadi nyakati hizi na zaidi.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |