2017-12-07 16:22:00

Papa kwa wakristo wa Taiwan:Ni kushuhudia matumaini yaliyomo ndani mwetu!


Kuna kazi nyingi ambazo kama wakristo tunaalikwa kutenda pamoja na kuhamasisha hadhi ya kila binadamu.Ni wito wa Baba Mtakatifu Francisko katika hotuba yake kwa wajumbe wa Baraza la Ushauri  la Taifa la Makanisa ya Taiwan , aliowapokea tarehe 7 Desemba 2017 katika Ukumbi wa Mkutano mjini Vatican.

Akitaja Injili ya Mtakatifu Yohane ,mahali ambapo anasema, “ kama mimi nilivyo wapenda ninyi, nanyi pendaneni,  kwa maana mkipendana, watu wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi awangu” (Yoh 13,34-35),anakumbusha kuwa,ili  upendo wa Mungu uweze kujikita kwa  dhati ndani ya maisha,  kila mkristo  anaalikwa kuwajibika kwa kushuhudia mbele ya ulimwengu, matumaini ambayo yamo ndani mwetu .
Na ndiyo maana ya ulazima na muhimu wa kutia jitihada hasa katika mahusiano kati ya imani za kikristo na kutangaza Kristo, hata kwa njia ya matendo ya upendo, hasa zaidi juu ya mipango ya mafunzo kwa vijana endelevu, kwa namna ya pekee kwa njia ya kuwafundisha mazungumzo ili kuweza kuunda jamii yenye haki.

Baba Mtakatifu anasema, Kanisa, tangu kuundwa kwa Baraza  la Ushauri la Taifa kwa ajili ya Makanisa ya Taiwan mwaka 1991, limejikita katika kuhamasisha kwa namna ya pekee umoja kati ya waamini, katika Bwana na kuongeza jitihada za mashusiano kati ya imani za kikristo.
Na mwisho wa mkutano, kabla ya kuwaalika kusali kwa pamoja sala ya Baba Yetu, ameeleza matumaini yake na shahuku ya kutaka kutembea kwa pamoja katika upendo mkuu ili  kuelekea siku ile ambayo Bwana Yesu anapenda kuwaona wote wanakuwa wamoja na ili dunia ipate kuamini!

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.