2017-11-21 15:37:00

Ujumbe wa Papa kwa njia ya Video kwa waamini na raia wa Bagladesh!


Baba Mtakatifu Francisko kama alivyo fanya kwa nchi ya Myanmar katika tukio la  ziara yake ya kitume ambayo inakaribia, vilevile ametuma ujumbe wake kwa njia ya Video kwa waamini na raia wa nchi ya  Bangladesh mahali ambapo anatarajia kufanya ziara ya kitume tarehe 30 Novemba hadi 2 Decemba 2017.

Katika ujumbe huo, Baba Mtakatifu anasema, wakati akijiandaa kutembelea nchi ya  Bangladesh siku chache zijazo, anatamani kuwatumia ujumbe wa salam za upendo wa kwa watu wote; ambapo ni matarajio yake kuwaona na kukaa pamoja nao.
Ainafika kama mtumishi wa Injili ya Yesu Kristo, kutangaza ujumbe wa mapatano, msamaha na amani. Kufika kwake ni kutaka kuwaimarisha jumuiya katoliki ya  Bangladeshi katika imani na ushuhuda wa Injili ambayo inafundisha hadhi  ya kila mme na mke na kuwaalika wafungue mioyo yao kwa ajili ya wengine hasa kwa walio maskini na wahitaji.

Wakati huo huo aidha, anatamani kukutana na watu wote kwa namna ya pekee kukutana na viongozi wa dini  huko Ramna. Baba Mtakatifu anaongeza, kwa sasa tunaishi kipindi ambacho waamini na wote wenye mapenzi mema kwa kila sehemu wanaitwa kuhamasisha kwa pamoja uvumilivu, heshima na kusaidiana mmoja na mwingine kama vile watu walio ndani ya familia moja ya kibinadamu.
Kadhalika Baba Mtakatifu anao utambuzi ya kwamba watu wa Bangladesh wako katika  jitihada kubwa za kufanya maandalizi makubwa  ya kumpokea, kwa njia hiyo anawashukuru! Anawaomba kila mmoja kusali ili siku ambazo atakuwa katika ziara hiyo ziweza kuwa kisima cha matumaini na kutiwa moyo kwa wote. Na juu yao wote na familia anawabariki kwa baraka ya Mungu yenye furaha na amani.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.