2017-11-09 10:35:00

Utambuzi wa Uadilifu wa Mtumishi wa Mungu Papa Yohane Paulo I


Tarehe 8 Novemba 2017 Baba Mtakatifu Francisko amekuta na Kardinali Angelo Amato, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kuwatangaza Wenye heri na Watakatifu. Katika Mkutano wao, amekubali maombi  ya kutambuliwa  kuwatangazwa wenyeheri na watakatifu wafuatao: 

Mtumishi wa Mungu Giovanni Brenner, Padre wa jimbo. Alizaliwa tarehe 27 Desemba 1931  huko Szombathely (Ungheria) na kuwawa kwa ajili ya kutetea imani yake tarehe 15 Desemba 1957.

 Mfadini Mtumishi wa Mungu Leonella Sgorbati, mwanashirika la Kimisionari wa Konsolata. Alizaliwa 9 Desemba  1940 huko  Rezzanello ya  Gazzola (Italia)  na kuwawa kwa ajili ya kutetea imani yake tarehe  17 Septemba 2006 huko Mogadishu (Somalia). Utambuzi wa uadilifu wa mwenyeheri Bernardo di Baden, Marchese di Baden; aliyezaliwa kati ya mwa mwaka 1428 na 1429 huko  Hohenbaden (Ujerumani)  na kifo chake tarehe 15 Julai  1458 huko  Moncalieri (Italia).

Utambuzi wa uadilifu wa  mtumishi wa Mungu Papa  Paolo I (Albino Luciani). Alizaliwa tarehe 17 Oktoba  1912 huko Agordo (Italia) na kifo chake tarehe 28 Septemba 1978 katika nyumba ya Kitume Vatican.

Utambuzi wa uadilifu wa Mtumishi wa Mungu Gregorio Fioravanti, Padre wa Shirika la Ndugu Wadogo wa Mtakatifu Francisko na Mwanzilishi wa Shirika la Watawa wa Kimisionari wa Moyo Mtakatifu.  Alizaliwa huko Grotte ya Castro (Italia)  tarehe 24 Aprili 1822 na kifo chake huko  Gemona (Italia) tarehe  23 Januari 1894;

Utambuzi wa uadilifu wa Mtumishi wa Mungu Tommaso Morales Pérez,  Padre wa Shirika la Wajesuit na Mwanzilishi wa Taasisi  katoliki za  Kilei  za Cruzados na Cruzadas de Santa María; Alizaliwa huko Macuto (Venezuela) tarehe  30 Oktoba  1908  na kifo chake tarehe  1° Oktoba 1994 huko  Alcalá de Henares (Hispania);

Utambuzi wa uadilifu wa Mtumishi wa Mungu  Marcellino da Capradosso, Msekulari wa ndugu wadogo wakapuchini . Alizaliwa tarehe 22 Septemba  1873 huko  Villa Sambuco ya Castel  ya Lama (Italia)  na kifo chake  tarehe 26 Februari  1909 huko Fermo (Italia);

Utambuzi wa uadilifu wa  Mtumishi wa Mungu  Teresa Fardella mjane wa Blasi, Mwanzilishi wa Shirika la watawa wa Kike wa Wana wa Maria Mtakatifu,  aliyezaliwa huko New York (Marekani)  tarehe 24 Mei 1867  na kifo chake  tarehe  26 Agosti  1957 huko  Trapani (Italia).

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.