2017-11-08 09:02:00

Baba Mtakatifu Francisko amekutana na Prof.Ahmad Muhammad Al-Tayyib


Tarehe 7 Novemba 2017 Baba Mtakatifu Francisko amekutana katika ofisi binafsi ya Ukumbi wa Mwenye heri Paulo VI Imam  Mkuu wa Al- Azhar, Profesa Ahmad Muhammad Al-Tayyib na wajumbe wake.

Hii ni kwa mara ya tatu Baba Mtakatifu Francisko kukutana na Kiongozi wa Kiislam wa Suuni  ili kujadiliana naye. Mara ya kwanza ili kuwa mnamo tarehe 23 Mei  2016 mjini Vatican, na mara ya pili mjini Cairo Misri tarehe 28 Aprili 201 , wakati Baba Mtakatifu aliposhiriki tukio la Jukwaa ya Amani huko Al Azhar akiwa katika ziara yake ya kitume nchini Misri.

Kwa upande wa wote wawili, tukio la kukutana limekuwa la muhimu hasa katika  kujadiliana zaidi juu wa wajibu wao pamoja  wa kujikita katika mchakato wa  amani dhidi hali za kisasa zinazoendelea kuibuka za kiitikadi kali za kidini na ugaidi.

Sr Angela Rwezaula 
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.