Tarehe 7 Novemba 2017 Baba Mtakatifu Francisko amewateua Makatibu wasaidizi wa Baraza la Walei na familia na Maisha. katika kitengo cha Maisha Amemteua Profesa Gabriella Gambino ambaye hadi kuteuliwa kwake alikuwa mwanachama katika kitengo cha Falsafa na Mtafiti, pia profesaa wa Falsafa na Sheria katika Chuo Kikuu cha Torvegata Roma. Pia alikuwa amekabadhiwa katika Taasisi ya Taalimungu ya Yohane Paulo II katika mafunzo ya Sayansi ya Ndoa na Familia .
Na kwa upande wa Kitengo cha Waamini Walei ameteuliwa Profesa Linda Ghisoni. Hadi kuteuliwa kwake alikuwa ni hakimu katika mahakama ya mchakato wa utenguzi wa ndoa kwa Mkoa wa Lazio kwenye Jimbo Katoliki la Roma, pia mkufunzi wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Roma tre.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |