2017-10-26 16:27:00

Papa:Chuo Kikuu Katoliki kinatoa thamani ya kutafuta ukweli kwa njia ya tafiti


Uhuru wa mtu unaharibika unapojikabidhi katika nguvu kiziwi cha dhamiri  na hasa ya kutaka kupata  mahitaji ya haraka na ubinafsi. Ni maneno ya Baba Mtakatifu Francisko katika hotuba yake kwa lugha ya kihispania  kwa jumuiya  Chuo Kikuu Katoliki cha Kireno, alipokutana nao asubuhi ya tarehe 26 Oktoba 2017 katika tukio la mwaka wa 50 wa kuanzishwa kwake.

Baba Mtakatifu ansisitiza hayo akikumbuka waraka wake wa “Laudato si “ Sifa kwa Bwana ya kwamba ni ujumbe wazi ambao uweze kuendelea kukua bila kuwa na zana ya kuuzuia. Hiyo ni kwasababu ya kuzingatia mafikiano ya kikundi ambacho kinakosa uamininfu na maadili ya thabiti , utamaduni, tasaufi ya kweli inayoweza kutoa kweli uthibiti na kutunza utawala wake binafsi.

Kwa njia hiyo Baba Mtakatifu ametoa swali muhimu ya kwamba je tunawasaidiaje wanafunzi wetu wasione shahada ya chuo kikuu kama vile ni pesa kubwa au ufahari mkubwa wa kijamii?  Sio ulinganifu huo tu bali hata kujibu swali jingine ya kwamba, ni muhimu kuwa thabiti. Ukweli wa kuwa mkatoliki Baba Mtakatifu anaongeza ni kipengele  kisichohukumu  Chuo Kikuu. Kinyume chake, kinatoa thamani kubwa, kwa upande huo anakumbusha hasa hatua ya Waraka wa  Kitume  wa Mtakatifu Yohane Paulo wa II juu ya vyuo vikuu Katoliki.Waraka  wake umeandikwa kuwa, msingi wa Chuo Kikuu ni jitihada za kutafuta  ukweli kwa njia ya utafiti, kuhifadhi na mawasiliano ya ujuzi kwa manufaa ya jamii”.

Inaweza kuzingatiwa kuwa, mafundisho ya chuo kikuu hufanya hitimisho lake katika imani anasema Baba Mtakatifu,  Lakini mafundisho Katoliki, hayazungumzi kama mwakilishi wa imani, lakini juu ya yote kama shahidi halali kwa sababu ya maadili. " 
Hatimaye Baba Mtakatifu  anakumbuka mwisho nini  maana ya chuo kikuu Katoliki pia na nini mana ya kuwa Mreno. Anasema, maswali ya watu wengi yanatufanya kutafakari juu ya  mapambano yao, ndoto na wasiwasi ya kwamba vyote hivyo vina thamani kubwa ambayo hatuwezi kupuuza. Bwana alikuja ndani ya ulimwengu na kwa njia hiyo, hatuwezi kupata uokovu nje ya ulimwengu wetu halisi.

Sr Angela Rwezaula 
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.