2017-10-20 15:34:00

Papa:Mataifa yanaalikwa kutafuta maslahi kwa ajili ya raia wake wote


Tarehe 20 Oktoba 2017, Baba Mtakatifu amekutana na  Wanachama wa Taasisi ya Sayansi jamii na  ubunifu wanaoshiriki katika mkutano wa mafunzo, pia hata taasisi zinazo wasaidia katika utafiti huo. Baba Mtakatifu anasema mafunzo hayo ni muhimu kwenye kipindi cha sasa cha dharura ili kuweza kujikita katika kutafuta na kubuni mbinu mpya za mshikamano katika soko, serikali na jamii ya umma ule  uhusiano wa kukabiliana na changamoto za nyakati zetu. 

Taasisi ya Yohane Paulo II iliundwa kwa lengo la kuhamasisha mafunzo na maendeleo ya Sayansi jamii, uchumi, siasa na sheria, ili kuweza kusaidia mambo msingi ya kutumia katika mafunzo na  katika maendeleo ya mafundisho jamii ya Kanisa. Taasisi hiyo pia ina kazi ya kutafakari  juu ya kuweka mafundisho jamii ya sasa. Kwa mujibu wa Baba Mtakatifu anaonesha kuwa ipo wasiwasi hata leo hii katika masuala makuu mawili msingi yanayosababisha kuongezeka ukosefu wa haki na ubaguzi wa maisha ya binadamu aliye pembezoni.

Ya kwanza anasema, ni ongezeko kubwa na  mkakati  wa  kutofautiana na unyonyaji wa sayari  kwa kiasi kikubwa kulinga  na ongezeko la umaskini na matajiri. Hata hivyo yeye binafsi anasema,  ukosefu wa usawa na unyonyaji sio uharibifu wala suala ambalo linajtokeza  mara kihistoria.  Siyo uharibifu kwasababu unasababishwa na mienendo tofauti kibinafsi na  hata sheria za kiuchumi ambazo jamii uamua kutoa.

Sababu nyingine ya pili ni  ile inyaohusu kazi isiyo faa kwa maisha ya binadamu. Anabainisha kuwa, kama jana Hati ya Kitume ya Rerum Novarum ya mwaka (1891), ilikuwa inatoa wito juu ya "bidhaa za haki" kwa ajili ya wafanyakazi. Leo hii  bado kuna dharura kama ile ile ambapo ni suala la  kujiuliza kwa nini haikuwekwa kwenye  matendo kwa kile kilichoandikwa katika Waraka wa Mwanga wa Mataifa (Gaudium et spes) isemayo ni muhimu kukabiliana na mchakato mzima wa uzalishaji na mahitaji ya mtu na aina zake za maisha (n.67) Baba Mtakatifu nasema kuongezea tena Hati ya Kitume  kuhusu “Sifa kwa Bwana ”(Laudato si) inayohusu mazingira kwa kuzingatia kazi ya uumbaji ambayo ni mazingira ya nyumba yetu .

Kwa  mtazamo wa sehemu ya pili inayohusu ubaguzi wa kijamii , Baba Mtakatifu anatoa wito  kuwa makini katika ulimwengu wa kazi ili kuweza kuwapo nafasi wazi, aidha kuwapo watu wenye uwezo wa kutengeneza mahusiano. Anawaalika kutoa vikwazo vitokanavyo na shinikizo  la umma au  kibinafsi  ili kuweza kutetea maslahi ya sekta mbalimbali pia umuhimu wa kuondoa  aina za uvivu kiroho. Hiyo  inahitaji hatua za kisiasa zijikite kiukweli katika huduma ya binadamu kwa  manufaa ya wote na heshima ya asili anasisitiza Baba Mtakatifu.

Maadili msingi kama vile demokrasia, haki, uhuru , familia, uumbaji haviwezi kutolewa sadaka na kuwa kama fadhili ya ufanisi , kwa kuwa njia pekee inathibitisha kwamba ni ustaarab wa soko. Baba Mtakatifu anabainisha: nchi au taifa, haliwezi kutambuliwa kuwa ni mmliki kwa manufaa ya wengine iwapo  hairuhusu miili raia au jamii kuingilia kati na kujieleza kwa uhuru na kwa nguvu zao zote. Hii ni kuvunja kabisa  msingi ambayo ni pamoja na mshikamano unaofanya nguzo muhimu ya mafundisho jamii ya Kanisa. Kwa njia hiyo Baba Mtakatifu anaonesha kuwa hapo kuna changamoto, jinsi gani ya kupatanisha haki ya mtu binafsi na ile ya faida kwa wote.

Mwisho anaonesha kutazama jukumu maalum ya vyama vya kiraia: kwamba, jukumu maalum la vyama vya kiraia ni kama kulinganishwa na kile cha  Charles Péguy aliyejikita katika karama ya matumaini: kama dada mdogo  kati ya fadhila nyingine mbili  ya imani na upendo ikishikana mkono na kuvuta mbele yao. Kwa namna hiyo Baba Mtakatifu anasema jamii ya raia inapaswa kuvuta kwenda mbele ya serikali na soko ili kuweza kufikiri  kwa upya sababu ya kuwepo na njia  zao za kufanya kazi .

Sr Angela Rwezaula 
idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.