Bwana atupatie neema ya kutambua ukweli ndani, kwa maana msamaha wa kweli wa Mungu ni wa bure unaotokana na neema na utashi wake, hautokani na na nguvu zetu binafsi na kazi ya kibinadamu. Ni maneno ya Baba Mtakatifu Francisko akifafanua Liturujia ya Neno la Mungu kutoka katika Barua ya Mtume Paulo Kwa Waroma, asubuhi ya tarehe 20 Oktoba 2017 katika Kikanisa cha Mtakatifu Martha mjini Vatican.
Matendo yetu mema ni jibu la upendo wa bure wa Mungu ambaye anasamehe daima na kufanya tuwe na haki. Utakatifu wetu ni ule wa kupokea daima msamaha na ndiyo maana zaburi ya siku inasema , heri aliyesamehewa dhambi, na kusitiriwa makosa yake. Heri Bwana asiyemhesabia upotovu, ambaye rohoni mwake hamna hila. Baba Mtakatifu anasema ni Bwana anayesemehe dhambi ya asili na ambaye anasemehe mara tu tunapomgeukia na kutubu kwakwe. Hatuwezi kusamehewa dhambi kwa nuzvu zetu wenyewe, bali ni yeye anasemehe,sisi tunaweza kujibu msamaha huo kwa ajili ya matendo yetu mema.
Jilindeni na chachu ya Mfarisayo, ambayo ni unafiki. Lakini hakuna neno lililositirika
ambalo halitafunuliwa,wala lililofichwa ambalo halitajulikana. Basi,yoyote mliyosema
gizani yatasikiwa mwangani; na mliyonena sikioni mwa mtu katika vyumba vya ndani,
yatahubiriwa juu ya dari.
Katika Injili ya siku kutoka Luka, Baba Mtakatifu anafafanua,aksema Yesu anatuelekeza
kutambua njia nyingine ya kutafuta haki, akitumia picha ya wale wanaojidai kuwa watakatifu
na kumbe ni wanafiki, ndani ya mioyo yao, papa nasema, ni wachafu ndani ya mioyo yao,
lakini kijujuu wanataka wanaonekane wenye haki na wema, wanafunga, wanasali au kutoa
sadaka. Lakini ndani ya mioyo yao hakuna kitu, wanaishi maisha ya kinafiki, hakuna
ukweli wowote ndani ya mioyo yao.
Baba Mtakatifu anabainisha kuwa watu hawa wanaishi roho ya kinafiki na kutafuta
utakatifu wa kinafiki : Yesu anawaalikwa watu waishi maisha ya kweli yaani ukweli
ukweli wa ndani. Kujihesbu mwenye haki ya kijujuu ni sawa na mapovu ya sabuni ambayo
leo hii yapo na kesho hayapo tena.
Yesu anataka tuwe na uwiano sawa kwa maana ya maisha ya kile tunacho fanya na kile
tunachoishi ndani ya roho zetu. Uongo na unafiki uharibu mtu vibaya sana, kwa njia
hiyo ni vema kujiuliza na kutubu maovu mbele ya Mungu wako. Hiyo ni tabia mbaya ambayo
taratibu inajengeka na kufikia hatua za kuwadhuru wengine. Kutubu binafsi kwa Mungu
wako ndiyo njia nzuri ya kuhepukana na unafiki na kujifunza hekima ya kujihukumu
binafsi bila kuficha dhambi zako mbele ya Mungu.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |