Mara baada ya Katekesi yake, Baba Mtakatifu amewakaribisha kwa namna ya pekee wawakilishi wa Catritas Internatinalis katika uzinduzi rasmi wa Kampeni ya kushikirishana safari . Baba Mtakatifu anasema kauli mbiu ya kampeni yao ni jina zuri ambayo amependelea iwe sambamaba na katekesi hiyo. Amewakaribisha wahamiaji, wanaomba hifadhi na wakimbizi ambao pamoja na Caritas ya Italia na Taasisi mbalimbali katoliki kuwa ni ishara hai katika Kanisa. Wanatafuta kuwa wazi na kujufungua wazi kwa wale walio baguliwa na kuwakaribisha.
Anawashukuru kwa jitihada zao za huduma bila kuchoka. Katika jitihada za kila
siku anaongeza Baba Mtakatifu, wao wanakutana na Kristo mwenyewe anaye wakumbusha
kwa namna ya pekee, kuwa karibu na ndugu kaka na dada kwa kufungua mikono wazi.
Maana mikono ikiwa wazi na hakika ni kama izile nguzo zilizozunguka uwanja wa Mtakatifu
Petro zikiwakilisha Kanisa mama linalokumbatia wote na kushirikishana safari ya pamoja.
Baba Mtakatifu aidha anawakaribisha wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali za jamii
ya umma wakijihusisha katika kuwatunza wahamiaji na wakimbizi, pamoja na Caritas ambao
pia wamekusanya sahini nyingi za kampeni ya sheria mpya ya wahamiaji katika mantiki
ya hali halisi ya sasa.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |