2017-09-27 15:49:00

Papa: Matumaini kama aina ya wema mwingine duniani ina maadui wake


Leo hii ninapendelea kuongelea juu ya maadui wa matumaini, kwasababu matumaini kama kila aina ya wema wa ulimwengu huu yana maadui wake.
Wakati wa maandalizi ya katekesi nimeijiwa wazo la historia ya kizamani ambayo chungu kilifunguka ikatokeza balaha kubwa la kihistoria katika ulimwengu. Lakini watu wengi  wanakumbuka sehemu ya mwisho ya historia hiyo ambayo inayofungua mwanga, kwamba mara baada ya ubaya wote kutoka mdomo wa kile chungu, zawadi ndogo ilijitokeza na kushinda ubaya wote uliokuwa umesambaratika . Pandora ambaye  mwanamke aliyekuwa analinda chungu hicho aliigundua hiyo mwishoni  yaani wagiriki waliita  Elpis ikiwa na  maana ya matumaini.

Ni maneno aliyo anza nayo Baba Mtakatifu Francisko wakati wa Katekesi yake ya Jumatano tarehe 27 Septemba 2017 katika uwanja mkubwa wa Mtakatifu petro mjini Vatican. Akiendelea, historia hiyo  ni muhimu kwasababu ya binadamu katika matumani. Watu wamezoea kusema palipo na maisha kuna matumaini , lakini ni kinyume na mawazo hayo, kwani anasema, ni matumaini yanayosimamisha miguu, yanalinda, yanatunza na kukuza. Iwapo binadamu hasingeweza kukuza matumaini, ina maana binadamu hasingeweza kuwa na fadhila hii, asingeweza kutoka katika shimo la andaki , aidha hasingeweza kuacha alama yoyote ya historia katika dunia hii.

Mshahiri mmoja wa kifaransa, Baba Mtakatiu naendelea Charles Péguy ameacha kurasa zake nzuri za matumaini. Kwa maana katika shahiri lake anasema Mungu hatoi mshangao tu wa imani  ya kuwa mwanadamu,  hata katika upendo lakini kile kitoacho mshangao wa hajabu ni matumaini: kwa wale watoto wasikini ambao wanaona mambo yanavyokwenda wanaamini kwamba kila kitu kitaenda vema kesho yake. Aidha anasema, mshahiri huyo anatoa mwaliko wa kutazama nyuso za watu wengi wanaopitia katika dunia hii, wazalendo, masikini wafanyakazi , wahamiaji watafutao maisha bora ya baadaye, ambao wanapambana kila siku pamoja na uchungu wa maisha magumu ya leo , wakiwa na majaribu ya kila aina, lakini ndani ya mioyo yao ni watoto ambao wanamatumani ya kupata  maisha mapya yenye haki na utulivu.

Matumaini ni msukumu wa moyo kwa yule nayesafiri kuacha nyumba, ardhi , wakati mwingine familia na ndugu kwa ajili ya kutafuta maisha bora, yenye hadhi kwa ajili yake na ndugu zake. Vile matumaini yanatoa msukumo wkatika mioyo ya yule anayepowakea, akiwa na shahuku ya kukutana, kujuana na kuzungumza . Matuamani ni msukumo wa kushirikishana safari ya maisha kama inavyokumbusha leo hii Kampeni ya Caritas ambayo leo hii inazinduliwa rasmi. Baba Mtakatifu anasema ndugu wote wasiogopte kushirikishana safari!. Daima  safari inafanyika kwa watu wawili : wale ambao wanakuja katika ardhi yetu, na sisi tunaokwenda katika nchi zao , ili kuweza kuwatambua tamaduni na lugha zao. Ni safari ya wawili , lakini bila matumaini safari hiyo haiwezekani kutendelea.Anasisitiza Matumaini ni msukumo wa kushirikishana katika safari.

Matumaini siyo wema wa watu waliojaza tumbo lao. Na ndiyo maana masikini daima wamekuwa mstari wa mbele katika matumanini. Na kwa maana hiyo tunaweza kusema ni masikini hata wale ombaomba na ndiyo wako mstari wa mbele katika historia. Ili Mungu aweza kuja duniani , alihitaji wao. Baba Mtakatifu anatoa mifano kwamba, tazama Yosefu na Maria, na wachungaji wa Betlehemu. Usiku wa Krismasi ya kwanza dunia yote ilikuwa imelalia utajiri  wake na mali zake, Wakati huo wanyenyekevu walikuwa wakiandaa kwa kimya mapinduzi ya wema. Walikuwa masikini wa kila kitu na waliishi kimasikini, lakini walikuwa na utajiri mkuu wa thamani ya kuishi katika ulimwengu huu  wakiwa hasa na utashi wa mabadiliko.
Baba Mtakatifu anasema, wakati mwingine kuwa na kila kitu katika maisha ni bahati mbaya. Fikirieni kijana ambaye hakufundishwa kuwa na karama ya subira  na uvumilivu, ambaye hajawahi kutoa jasho la jambo lolote, au ambaye ameunguza hatua zake zote kabla ya kufikisha miaka 20, anatambua  dunia ya leo inakwendaje. Hii ina maana ya hatari, kwa maana umefungia mlango wa shahuku na ndoto, utafikiri ni kijana lakini ndani ya moyo wake amekwisha shuka katika kipindi cha vuli. 

Baba Mtakatifu anfafanua, kuwa na moyo mtupu ni kizingiti kikubwa cha matumaini. Ni hatari  dhidi ya matumaini katika safari ya   maisha ya kikristo.
Iwapo Mkristo anakumbana na hali hiyo, lakini anatambua namna gani ya kupambana nayo. Mungu amemuumba kwa sababu awe na furaha tele na aondokane na  mawazo ya ubaya. Ndiyo maana kuna haja ya kuulinda moyo dhidi ya vishawishi, dhidi ya furaha ambayo kiukweli vishawishi hivyo havitoki kwa Mungu. Iwapo vinaweza kujitokeza ndani ya moyo ukawa na machungu, basi  tunaweza daima kukimbilia jina la Yesu . Tunaweza kurudia sala rahisi ambayo inapatika katika Injili isemayo Bwana Yesu Kristo Mwana wa Daudi unihurumie mimi dhambi. Ni sala nzuri yenye kuwa na matumaini ya kwamaba na mwekeza Yesu amabaye ana uwezo wa kufungua milango na ya kutoa suluhisho la matatizo na kufanya utazame upeo wa matumaini.
Sisi si peke yetu katika kupambana dhidi ya kukata tamaa. Yesu aliushinda  ulimwengiu na anaweza kushinda ndani mwetu iwapo tutakimbilia katika wema. Iwapo Mungu yupo nasisi hakuna anayeweza kuiba ile fadhila ambayo sisi tunahitaji ili kuishi, na hakuna anayeweza kuiba matumaini anasema Baba Mtakatifu.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.