2017-09-12 15:46:00

Kard. Baldisseri:Sinodi ya Vijana 2018 ni Sinodi ya vijana wote


"Natoa salam  kwenu wote maprofesa  na vijana ambao kwa furaha kubwa Sekretarieti Kuu ya Sinodi ya Maaskofu  inawakaribisheni katika mwanzo wa Semina  ya Kimtaifa ya mafunzo kuhusu hali halisi ya Vijana, iliyoandaliwa kwa malengo ya maandalizi ya Sinodi  ya XV ya Kawaida ya Maaskofu itakayo kauli mbiu “Vijana, Imani na maang’amuzi ya miito”. Ni maneno ya Kardinali  Lorenzo Baldisseri, Katibu Mkuu wa Sinodi ya Maaskofu aliyoanza nayo wakati wa ufunguzi wa Semina ya Kimataifa kwa maprofesa na wawakilishi wa Vijana kutok  Mabara matano, kwa lengo la maandalizi ya Sinodi kuhusu vijana 2018 na  semina hiyo imaeanza tarehe 11 hadi 15 Septemba mjini Vatican.

Kardinali Baldisseri anasema, ni zaidi ya miaka hamsini ya shughuli hizi ambapo Sinodi imeundwa kwa mantiki ya aina yake ambayo ina utajiri mkubwa kutokana na  mafundisho ya Mtaguso wa II wa Vatican na kwa namna ya pekee  umekuwa kiungo  na kuimarisha zaidi sura ya Kanisa leo hii. Sinodi ya Maaskofu mwaka  2018 haiwakilishi jambo la kushangaza zaidi ya kuwakilisha  ujumbe wa mwisho wa Mtaguso wa binadamu  ambao uliwalenga vijana, maana  mababa wa  mtaguso walikuwa na lengo na  mawazo ya kuwakabidhi Vijana  usukani wa Kanisa la baadaye.
Ujumbe wa mababa ulikuwa unasema:”Ni nyinyi vijana wa dunia nzima ambao mtaguso unawalekeza ujumbe wake wa mwisho. Ni nyinyi ambao mnaupokea mwenge huo katika mikono yenu kutoka kwa mababa ili uwezea kuangaza dunia katika kipindi cha mabadiliko ya kihistoria. Ni nyinyi ambao mnapokea vema  mifano na mafundisho ya wazazi wenu, walimu wenu na kuunda jamii endelevu: Kwa maana ni nyinyi mtakao okoa au kupotea ndani yake”.

Kwa miaka minne Kanisa linafanya kazi kwa ajili ya kudumisha na kukuza uso wake uwe bora kulingana na ishara za mwazilishi wake, yaani yule anaiyeishi ambaye ni Kristo daima kijana. Na baada ya  kutazama kwa upya maisha yake, mababa  wanawageukia kwamba ni nyiny vijana hasa katika mtaguso wake  ulitoa mwanga na kuangaza wakati ujao na wakati wenu endelevu. Kanisa ambalo linalotamani kuona  jamii inayo wazunguka  kuijenga na kuheshimu hadhi yake, uhuru wake , haki za watu  ambao ni nyini wenyewe. Kardinali Baldisseri anasema, maneno ya  mababa wa mtaguso yote yanabaki hata leo ya kufaa  kwasababu bado ni bahati na fursa ya njia ya Kanisa na zaidi katika muhongo wa  mabadiliko tunayoishi kwa wakati huu. Kwa njia hiyo mwaka kesho mababa wa Sinodi wataunganika Roma na Petro chini ya Petro , kutafakari pamoja juu ya suala la utume wa  kichungaji kwa kizazi kipya, kwa kutambua vema na  akili yake ya ufunguo wa somo uliotolewa na Baba Mtakatafu Francisko, akiwataka mababa wa sinodi wajikite zaidi kwa namna ya pekee katika imani na maang’amuzi ya vijana.

Kwa upande wa mantiki ya Semina, inawapa fursa ya kuchangia na kuwaruhusu watazame  vema na kupiga picha ya hali halisi ya vijana katika kugundua na kutambua sifa msingi zinazowashirikishwa na vijanale wakati huo huo kwa kuzingatia wingi wa mazingira ya kijiografia na utamaduni,na idadi kubwa ambayo uwafanya dhana ya vijana .Mwisho wa seminari hiyo ambao siyo tu kwa lengo la  mkutano wa  wa kimataifa, bali hata ni fursa  ya nafasi nyingi iwezekanavyo ya kufanya  mahusiano kati ya wataalamu kutoka katika mabara yote, lakini pia ni kuhamasisha na kukuza mazungumzo na viongozi katika taaluma mbalimbali ya elimu jamii, saikolojia , uchumi, komputa , falsafa na taalimungu  ya huduma ya kichungaji.
Zaidi ya wataalamu waliopo, hawakosekani wawakilishi wa vijana wenye ujuzi , waliotambuliwa kwa ushirikiano  wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Walei, familia na maisha. Hawa ni wajumbe wa huduma ya kichungaji kwa vijana katoka katoka mataifa mbalimbali na makanisa mahalia , aidha Shirikikisho la wanachama  Vijana na  Wawakilishi  vyama vya kitume vya  Wanafunzi.

Katika mahubiri ya Baba Mtakatifu Francisko kwenye maandalizi ya Siku ya vijana  duniani mwaka huu kwenye Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria Mkuu alisema: Katika  sinodi ijayo kuwa hakuna kijana yoyote ambaye ajisikie kubaguliwa , na wakati huo sinodi ya vijana siyo kwa ajili ya wakatoliki tu, bali ni sinodi ya vijana wote ambao ndiyo wako mstari wa mbele. Kwa njia hiyo sinodi ni kwa ajili ya vijana wote, wavivu , wasio kuwa na imani walio na imani, walio mbali na Kanisa , wasio mjua Mungu, wote ni lazima kusikilizwa, kwa maana kila kijana analo jambo la kusema kwa wengine wakubwa kwa wadogo, mapadre , watawa na maaskofu na papa mwenyewe.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.