2017-09-09 09:16:00

Papa amesikitishwa na kifo cha Kard. Carlo Caffarra wa Bologna Italia


Baba Mtakatifu Francisko ametuma salamu zake za rambi rambi kutokana na kifo cha Kardinali Carlo Caffarra, askofu mkuu mstaafu wa Jimbo Kuu la Bologna aliye kuwa na umri wa miaka 79. Kifo cha Kardinali Carlo Caffarra kilitokea tarehe 6 Septemba Jimboni Bologna nchini Italia.
Kufuatiwa na kifo hicho, telegram ya  Baba Mtakafu kupitia kwa Askofu Mkuu Matteo Zuppi  wa Jimbo Kuu la Bologna anaonesha masikitiko yake na kushiriki uchungu na Jumuiya nzima ya Jimbo la Bologna na familia yake kuondokewa na mpendwa wao na Kanisa zima.

Akikumbuka maisha yake Kardinali Carlo Caffara, Baba Mtakatifu anaeleza  juu ya huduma yake ya kichungaji kwamba, aliitenda kwa uamninifu, furaha na upendo wa kina kwa Kanisa. Ameonesha  juhudi yake pamoja na ukarimu wake wa kitume  hasa akiwa mstari wa mbele,  mwanzilishi na profesa wa Chuo cha Kipapa cha  Yohane Paulo II, katika mafunzo ya ndoa na familia. Baba Mtakatifu anaongeza, Kardinali Carlo amejikita sana katika  shughuli ya kitume bila kuchoka na kupenda sana Kanisa katika majimbo makuu ya Ferrara na Comacchio na baadaye kama kiongozi mwenye hekima na msimamo wa kuongoza majimbo makuu.

Mwisho Baba Mtakatifu anatoa maombi yake kwa njia ya Bikira Maria na Mtakatifu Petroni msimamizi wa Jimbo la Bologna ili Bwana apokee roho ya mwaamini na mtumishi wake kwenye kiti cha enzi hukoYerusalemu mpya.
Mazishi ya Kardinali Carlo Caffarra yatafanyika Jumamosi 9 Septemba saa tano asubuhi katika Kanisa Kuu Bologna nchini Italia.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.