2017-09-08 16:02:00

Gombera wapya katika Seminari Shirikishi za majimbo ya Camerun na Zimbawe


Kardinali Ferdinando Filoni Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Uinjilishaji wa watu tarehe 28 Juni 2017 alimteua Gombera  wa Seminari ya shirikisho la Majimbo ya Mtakatifu Josephine Bakhita na Majimbo  makuu ya Ngaundere  nchini Cameruni, Padre Andre Pekeu aliyekuwa Padre la Jimbo la Yagoua.

Gombera mpya alizaliwa tarehe 27 Mei 1974 katika kijiji ka Mindjil. Amefanya mafunzo ya falsafa na Taalimungu katika Seminari Kuu ya Maroua na  kupata daraja Takatifu la  upadre  tarehe 25 Juni 2005. Aliendelea na masomo yake ya usimamizi wa fedha katika Chuo Kikuu  Katoliki cha Afrika huko Yaounde. Baada ya kupata daraja la upadri alikuwa Paroko katika maparokia mbalimbali pia utume mwingine kama mchumi wa jimbo,huduma ya Kanisa dogo huko Codas – Caritas na Katibu msaidizi wa Askofu.

Hali kadhalika nchini Zimbabwe, Kardinali Filoni, tarehe 1 Juni 2017 alimteua Gombera mpya wa Seminari Kuu ya Shirikisho ya Majimbo Harare, Padre Andrew Lastborn Foto padre wa Jimbo la Masvingo. 
Gombera mpya alizaliwa tarehe 10 Desemba 1976. Baada ya shule ya msingi alijiunga na Seminari ndogo  ya Chikwingwizha  na baadaye kuendelea na Seminari Kuu kupata  diploma ya mafunzo ya Falsafa na Taalimungu.Aliendelea na mafunzo ya dini  katika Chuo Kikuu Zimbabwa 1997-2001 na kupokea daraja Takatifu la upadre tarehe 23 Juni 2003. Mnano mwaka  2005-2011 aliendelea na masomo ya uzamivu wa Biblia katika Chuo Kikuu cha Kipapa Urbaniano mjini Roma.


Katika maisha yake ya kichungaji amewahi kuwa paroko msaidizi katika jumuiya tofauti za  parokia na kusimamia Kanisa dogo katika shule na vyama vya kitume vya wanafunzi. Amewahi kuwa Katibu wa Askofu na tangu mwaka 2015 alikuwa Gombera wa Seminari ndogo ya Mt. Kizito pia muhamasishaji wa miito katika jimbo.

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.