Askofu Mkuu Ivan Jurkovič, mwakilishi wa Kudumu wa Vatican katika Umoja wa mataifa
ametoa hotuba katika kwa mashirika mengine ya Kimataifa huko Geneva katika Mkutano
wa 7 wanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa kupiga marufuku mabomu yenye kusababisha
maangamizi makubwa .
Ameanza kwa shukrani za dhati kumruhusu kutoa ujumbe wake kwa wakurugenzi wa ulimwengu
kwa jitihada zao zinazofanywa katika Mkutano wa Mkataba wa Kimataifa wa kupiga marufuku
mabomu yenye kusababisha maangamizi makubwa. Anathibitisha ushirikiano wao huo kuwa ,
hakuna swali la kujiuliza kwamba, tangu Mkataba wa Kimataifa wa kupiga marufuku mabomu
yenye kusababisha maangamizi makubwa kuanza kutumika ni mambo mangapi yametendeka
kwasababu, kumekuwapo michango ya pamoja na ushirikiano kati ya wadau mbalimbali na
imefanikisha maendeleo muhimu na kufanya utofauti halisi duniani, hasa kati ya waathirika
walioathirika pia miongoni mwao wale ambao wamesaidia kuzuia.
Hata hivyo,anasema, tunapoadhimisha mwaka wa 7 wa kujikita kwa nguvu katika mkataba
huo wa Kimataifa wa kupiga marufuku mabomu yenye kusababisha maangamizi makubwa, bado
kuna wito unaokumbusha nguzo hii kwamba inendelee kutumiwa katika badhi ya migogoro
mingine leo kwasababu kuna hatari za kuenea na kuongeza waathirika wapya. Ni lazima
kujikita zaidi katika mkatabu huo uliopitishwa kwani ni muhimu kushikilia wajibu wetu
wa kimaadili na kulinda heshima ya waathirika, kurudia kupiga marufuku chini ya Mkataba
kupitia mboni ya kibinadamu.
Sio tu kwamba suala la ulimwengu lemye kuwa na matokeo ya moja kwa moja juu ya uendeshaji
na utekelezaji wa Mkataba wa Kimataifa wa kupiga marufuku mabomu yenye kusababisha
maangamizi makubwa lakini pia njia ya kupunguza mabomu hayo yanyoe leta athari, ili
hata binadamu aweza kufurahia jitihada hizo za kimataifa katika kutekeleza Malengo
ya Maendeleo Endelevu kwa ufanisi zaidi.
Utekelezaji wa kimataifa kwa Mkataba huo kwa kuzingatia viwango vyake, utachangia kufikia maendeleo endelevu ya kawaida ya mwanadamu. Na hasa ufunguzi wa maeneo yaliyochafuliwa, ushirikiano wa kimataifa na usaidizi kwa waathirika ni muhimu kwa kufikia maendele endelevu ya 2030 na kuzuia majeraha ya baadaye. Askofu Mkuu Ivan anasema, Vatican bado ni thabiti katika kujikita na kuamua kuchangia ili kuleta ufanisi dhidi ya changamoto hii ya kibinadamu. Kwa njia hiyo ni wito kwa majimbo yote na nchi zote hata wale walio nje ya Mkataba huu ili kuzingatia kujiunga na jitihada za kimataifa katika kufikia lengo la wote pamoja katika kujenga zaidi dunia iliyo bora, salama na ushirikiano zaidi.
Amemaliza akisema,hebu tuongeze jitihada zetu mara mbili na tuwe na nia ya kuunga mkono ulimwengu huu katika utekelezaji kamili wa mkataba wa kupunguza mabomu ya maangamizi makubwa kama ilivyoelezwa katika mpango wa utekelezaji wa Dubrovnik na kuhakikisha kuwa, baadaye vituo vya makundi hayo haviwezi kuwa sababu ya mateso ya wanadamu. Tuna deni hili kwa waathirika wengi wa zamani na kuzuia waathirika wengine zaidi.
Ikumbukwe kwamba Mkataba wa Kimataifa wa kupiga marufuku mabomu yenye kusababisha maangamizi makubwa ulianza kutumia rasmi tarehe 1 Agosti 2010.Mabomu hayo yajulikanayo kama cluster yakilipuka hufuatiliwa na milipuko mingine kadhaa yenye uwezo wa kusababisha maafa katika maeneo makubwa. Wanaharakati wanaopinga silaha hizo wanasema mabomu hayo kwa kawaida yanashindwa kulipuka na kubaki hivyo kwa miaka kadhaa , na hivyo kuwa hatari kwa raia kwa muda mrefu baada ya mapigano kumalizika.Ni zaidi ya mataifa mia moja yaliyotia saini mkataba wa kupiga marufuku matumizi ya mabomu hayo. Lakini baadhi ya mataifa yenye nguvu duniani,na mengineyo kama vile Marekani, Urusi, na Pakistan na nyinginezo bado yamekataa kusaini mkataba huo, wakisisitiza kuwa silaha hizo kisheria zinaweza kutumika kwa shughuli za kijeshi.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |