Kardinali Kurt Koch kwa niaba ya Baraza la Kipapa la kuhamasisha umoja wa Wakristo na yeye binafsi anapenda kuwatumia salamu wote wanaoshiriki mkutano kuanzia kwa Patriaki Bartolomeo wa kwanza, Patriaki Theodros wa Alesandria na Afrika nzima, maaskofu wamonaki wakristo wawakilishi wa makanisa ya Kiorthodox na washirki wote katika mkutano huo wa XXV wa Kimataifa wa Tasaufi ya Kiorthodox. Kardinali Koch anasema katika kuadhimisha mwaka wa 25 wa Mkutano huo anapenda kumshukuru Mungu na kuwapongeza Jumuiya ya Monasteri ya Bose kwa kuanzisha tukio hili ambalo kwa miaka mingi sasa imekuwa muhimu katika mahusiano ya Kiorthodox na Wakatoliki; Pia yeye binafsi alivyo weza kufanya uzoefu huo mwaka jana alipoweza karibishwa mahali hapo. Kauli mbiu ya Mkutano huo ni zawadi ya kukaribishwa , ambapo anasema kuwa inatokana na moyo wa taufi ya kikristo.
Kwani hiyo siyo kwa bahati mbaya kuona kwamba ni Fumbo la imani ya kikristo na Utatu Mtakatifu ambao unawakilishwa na mgeni katika nyumba ya Ibrahimu , na ambayo wao wamechagua kama kauli mbiu ya mkutano huo. Katika ishara yake; Ibrahimu alifanya uzoefu wa kukaribisha mgeni,kwa njia hiyo ni binadamu anamkaribisha Mungu mwenyewe. Na hiyo ni kwasababu Yesu mwenyewe anasema anayenipokea mimi anapokea yule aliyenituma. Kwa ulinganifu wa makaribisho hayo ni kusema kwamba yule anayepokea anafanya uzoefu wa kukaribishwa na Mungu. Na ndiyo maana hiyo picha ya mgeni wa Ibrahimu haioneshi tu makaribisho ya binadamu, bali hata makaribisho ya Mungu.
Ni ishara ya umoja kwa maana ya ekaristi, mahali ambapo Utatu Mtakatifu unaalika
kila mmoja kushiriki umoja na Mungu. Katika Karamu ya milele kwa wale waliokombolewa,
Neno takatifu linasema; Bwana atajifunga mkanda kiunoni atawaketisha mezani na kuwahudumia.
Utatu Mtakatifu siyo jambo lisilokuwapo kwani ni mpango wa maisha ya kijamii .
Leo hii suala hili la kukaribisha ni changamoto kubwa katika milango ya jamii zetu
mahali ambapo watu wengi wanazidi kubisha hodi wafunguliwe maana wamelazimishwa na
kulazimika kuacha nchi yao.
Kardinali Koch anasema; mbele ya changamoto hizi, kwa mujibu wa maadili kama ilivyoandikwa na Max Weber, ineweza kufuata maadili ya aina mbili: maadili ya kukubali na maadili ya uwajibikaji. Siyo rahisi kudharau uchaguzi wa maadili mengine kwani kila maadili katika ngazi binafsi na hata kisiasa ni lazima kuwa sawa katika kuongozwa na msingi wa kukubali na kujikita kwenye uwajibikaji; mambo hayo mawili yanakwenda pamoja. Lakini ni jinsi gani ya kujikita katika kukubali na kuwajibika?:Kard, anatumia mifano hali a kuwa; Baba Mtakatifu Francisko, Patriaki Bartolomeo na askofu Mkuu Ieronymos katika hati yao ya pamoja iliyotia saini tarehe 16 Aprili 2016, walionesha kwamba uwajibikaji wa kweli hauweki kizingiti cha kukaribisha; badala yake ni kinyume kwasababu ni kufungua mikono wazi kukaribisha wengine na wakati huo huo ni kijibu mahitaji ya kesi nyingi za binadamu walizo nazo kutokana na kauacha nchi zao ili kutafuta maisha bora .
Pamoja na hiyo inayofanan nayo ni ile ya Papa na Patriaki Cyril katika waraka wao wa pamoja wa tarehe 12 Februari 2016, walikuwa wametoa wito wa kutafuta suluhisho la sababu zinazowafanya wahamiaji kuondoka katika nchi zao, hata tofauti za migogoro au zile za ukosefu wa ugawaji rasilimali katika dunia hii. Na hati hizi za hivi karibuni zinaonesha kweli suala la wahamiaji na makaribisho kwamba ni mada nyeti na msingi katika mahusiano kati ya wakatoliki na waorthodox kwa ujumla katika mahusiano ya kiekumeni. Kwa njia hiyo Kardinali anatoa shukrani zake kwa jumuiya ya kiekumene ya Bose kuandaa mkutano huo juu ya mada hiyo nyeti ambayo yeye binafsi anasema; ni fursa kubwa ya kuweza kubadilishana mawazo, wakati huo huo kuwawezesha washiriki wote kufanya uzoefu wa kindugu katika ukarimu wa kukaribisha na kupokelewa.
Vilevile mkutano huo unaweza kuwa fursa kwa wote wakatoliki na waorthodox kama ahujaji wa Emmau wakitembea pamoja na wajadiliana wakisindikizwa na Kristo. Na kama mitume wa Emmau katika safari hiyo ya pamoja wanaweza kukaribiana kila siku, siyo tu kutambuana bali katika kupokea pamoja mwili na dam ya Yesu Kristo pamoja katika umungu wake na undugu wa milele.
Sr. Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |