Shirika la Wasalesiani na Ofisi ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuthibiti madawa ya kulevya na kuzuia ualifu (Unodc) wanashirikiana pamoja kwa muda sasa kwa ajili ya kuwasaidia vijana barabara mjini Addis Abeba. Nia kubwa ni kuwapa mtazamo mpya wa maisha na kuwaondoa katika njia mbaya za unyonyaji, unyanyaswaji na ualifu wanaoufanya ili waweze kuishi . Ongezeko la watoto walioachwa peke yao na wengine kukimbia njaa ni janga kubwa linalo athiri jamii ya Ethiopia.Kwa njia hiyo Novemba 2015 Shirika la Mtakatifu John Bosco kwa kushirikiana na Ofisi ya umoja wa Mataifa ya kuthibiti madawa ya kulevya na kuzuia ualifu , walianzisha pamoja kituo cha kupokea na kuwasaidiwa waathirika wa migogoro ya ndani ya nchi hiyo kwa kufuta sheria.Tangu wakati huo vijana wengi wasichana na wavulana wanaishi katika kituo cha makaribisho cha Mpango wa watoto wa John Bosco chini ya uangalizi wa watawa wa Shirika hilo.
Taarifa kutoka kwa muhusika wa utume wa Kimisionari wa wasalesian kutoka New Rochelle,Marekani,
Padre Mark Hyde amesema,kwa upande wa mji wa Addis Abeba tu kuna watoto zaidi ya 100
elfu wanye kuwa na mahitaji ambao hawana msaada na wanaishi barabarani. Kutokana na
Kituo cha watotoJohn Bosco kuwa kimoja katika mji huo kuweka nafasi ya mapokezi
ni shida kubwa kukabiliana na kipeo hicho. Pamoja na hayo ushirikiano huo unajitahidi
kutoa chakula na vifaa vya elimu na mahitaji binafsi ili kuweza kuwasaidia idadi
kubwa iwezekenavyo ya watoto hao wadogo barabarani.
Hali kadhalika naye Mkurugenzi wa kituo hicho Andualem Tafesse, amesema kuna watoto
ambao wameachwa peke yao au kuuzwa na wazazi wao ambao baadaye wanaishia magereza
kutokanavitendo vya ualifu na wizi. Vijana wengine wanafanya ualifu makusudi wakitegemea
kwamba, kwenda magereza ndiyo njia ya kukidhi haja zao za mahiji msingi. Lakini watoto
hawa wanapo acha magereza hawana mahali pa kwenda, wanaishia tena barabarani. Hii
ni hali mbaya inayodi kuendelea na kuzidisha umaskini, na mahangaiko ya hapa na pale
, na sababu kubwa ya kujiingiza katika omba barabarani mkate wa kula kwa ajili ya
siku.
Katika kituo cha makaribisho, vijana hawa wanapata chakula, nguo za kuvaa , aidha kuwawasindikiza katika mchakato wa kisaikolokia na kuwapatia kozi ya mafunzo ya kusoma na kuandika. Wakiwa tayari ndipo wanaweza kuwaelekeza katika mwelekeo wa mafunzo ya ufundi mbalimbali kama vile ufundi ujenzi, magari, uselemala, kupika na kushona; kila mmoja kadiri ya uwezo alio nao. Kwa namna hiyo kituo hicho ni kwa ajili ya kuwasadia waweze kujitegemea wao wenyewe baada ya kutoka katika kituo hicho. Hiyo ndiyo lengo kuu la mafunzo ya kituo ambapo pia watawasaidia vijana hao kwa miezi mitano kiuchumi mara baada ya mafunzo wakati wakiendelea wenyewe kutafuta ajira na mahali pa kuishi kwa kijitegemea.
Hadi sasa matokeo ya vijana ambao wamepata kufaidika katika kituo hicho wanatoa
shukrani kwa kujitolea kushirikiana na wahudumu wa kituo kwenda usiku kuwatafuta vijana
wenzao wanaolala barabarani ili waweze kuja katika kituo hicho . Wanawatia moyo ili
waweze ufika na kusaidiwa na kituo hicho.
Mkurugenzi wa Kituo anamaliza akisema, wale ambao wanaishi katika barabara wanayo
shahuku ya kuweza kuishi katika jamii lakini wakati mwingine hawajuhi wafanye nini.
Hata hivyo anawashukuru sana wafadhili wengi na wadau wote wanao endelea kujikita
katika kuwezesha mradi wa kituo hicho cha vijana na hatimaye waweze kuona njia mpya
za maisha yao.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |