2017-08-17 15:33:00

Furaha ya Maaskofu wa Ufilippini kwa mswada wa Bungu kuhusu maskini


Kuridhika na kufurahi ni hisia ambayo Kanisa Katoliki la Ufilippini limeonesha wakati wa kupokea taarifa ya  kupitishwa kwa mswada wa bunge ya nchi hiyo wenye lengo la koboresha hali ya maisha ya maskini na wanyonge katika nchi. Kupitishwa kwa sheria hiyo unaweza kuifanya Serikali kutoa kipaumbele katika mipango inayojikita katika  maskini hasa sekta ya chakula, nyumba na maisha bora, elimu na afya.

Askofu Msaidizi wa Jimbo la Manila Broderick Pabillo,kuhusiana na rasimu ya Sheria hiyo ameilezea kwamba ni  kama moyo mkuu wa maskini, ni kipimo muhimu ambacho kinaonesha kutokusahau maskini,hivyo ni matumaini yake kwamba pendelezo hilo linaweza kuwa sheria  timilifu kwa mambo yote .
Kwa upande wa Padre Edwin Gariguez ambaye ni mwanachama wa Sekretarieti ya Taifa  kwa ajili ya shughuliza za Baraza la maaskofu mahalia, amesema, serikali inapaswa kutenda  kwa haraka iwezekanavyo ili kupunguza umaskini nchini humo.

Hiyo yote ni kutokana na taarifa za kusikitisha kuwa, janga la umaskini katika  nchi ya Ufilippini inakithiri kiasi kikubwa  zaidi cha kuwafanya watu wengi  wa Ufilippini kulazimika kuuza hata viungo vyao katika nchi tajiri za magharibi wanaotafuta kwa udi na ufumba matibabu. Kwa mujibu wa takwimu za serikali huko  Manila, inasadikika kuwa, ni watu karibia elfu tatu wamehusika katika miaka ya hivi karibuni kwenye biashara haramu ya kuuza viungo kinyume cha sheria.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.