Baada ya Madaktari wasio na Mipaka na Shirika lisilo la Kiserikali ya Ujerman (Sea
Eye), hata Shirika lisilo la Kiserikali la Saidia Watoto (Save the Children) limesimishwa
uendeshaji wa kokoa wahamiaji katika Bahari ya Mediterranea. Mashirika haya ya Kibinadamu
yako katika kutafakari zaidi mara baada ya tamko la kutoka Mamlaka ya Serikali nchini
Libia,ambapo wametaka kudhibiti na kuzuia Meli za mashirika yasiyo katika maji ya
kimataifa. Ni mahali ambapo hata meli nyingine zimesimama katika Kisiwa cha Malta
wakisubiri kujua hali ya usalama kabla ya kuendelae na operasheni zao.
Shirika la Saidia Watoto (Save the Children) wanalalamika kutokana na kulazimishwa
kusitisha operesheni hiyo ya kuokoa watu Bahari ya Mediterranea. Ujumbe unasema,
ni hali ya kusikitisha kwa sababu ya hatari ya usalama wa wafanyakazi na kwa ajili
ya uwezo wa hali ya Meli ya Vos Hestia kutekeleza uokoaji wake. Katika hali hii mpya,
Shirika la Kusaidia Watoto (Save the Children) inasema boti za wahamiaji watalazimika
kurudi Libya wakati huohuo watoto wengi na vijana watakufa kabla ya kuacha eneo jipya
la Sar ya Libia.
Mkurugenzi wa Uendeshaji, Rob MacGillivray anasema, Shirika la Kusaidia Watoto
liko tayari kuanza tena shughuli zake kuokoa eneo hilo, lakini wanawajibu wa kuhakikisha
usalama wa timu yao na ufanisi wa utendaji. Kabla ya kuweze kuendelea na operehseni
hiyo ni lazima kuwa na uhakika hasa juu ya usalama wa wafanyakazi wao amesema. Save
the Children pia wanao wasiwasi mkubwa kuhusu kupungua kwa uwezo wa nguvu za uokoaji
baharini kutokana na kusimamishwa kwa shughuli hata za mashirika mengine katika Mediterranea.
Anasema kuwa wao wanelewa na kuheshimu mashirika yote yasiyo ya kiserikali katika
hali hiyo ya kuchukua uamuzi mgumu ambao wanajikuta katika hali hiyo.
Amemalizia akisema, kusitishwa kwa uperesheni za meli katika kuokoa watu inahatarisha
maisha ya binadamu na kupunguza uwezo wa kuwasadia watu kwa njia hiyo ni muhimu kuanza
kwa upya operesheni hiyo mapema iwezekanavyo.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |