“Wahamiaji na wakimbizi wanastahiili kupewa hadhi yao”. Ndiyo taarifa iliyoandikwa na Askofu Vincent Long Van Nguyen mwanachama wa Baraza la Maaskofu wa Australia na mjumbe katika Sekta ya wahamiaji na Wakimbizi. Kauli ya maaskofu imewadia baada ya siku za hivi karibuni mkimbizi katoka kambi ya wakimbizi wa Manus huko Papua Guinea Mpya kukutwa amekufa na Mwauame mwenye umri wa miaka 31 akiwa na asili ya Iran ambapo mwili wake uliokutwa katika msitu karibu na kambi hiyo.
Ujumbe unasema,waliofika nchini Australia katika kutafuta usalama na maisha bora wanasahili zaidi wakati watu wanaotafuta hifadhi ndiyo wenye kuathirika katika jamii yetu ya kimataifa. Kwa njia hiyo ni muhimu kutoa kipaumbele na kuwashughulikia ili wapate hadhi yao na zaidi lazima wawe na huru wa kuchagua mahali wanapotaka kwenda katika nchi zenye usalama ambapo hakuna mateso.Katika barua hiyo wanatoa wito kwa serikali ya Australia kutoa huduma na msaada kwa wale wakimbizi wanaoishi katika kisiwa cha Manus wakisubiri ufumbuzi hadi sasa.Hata hivyo wanadai pia serikali ipitishe mpango wa ulinzi kwa ajili ya wahamiaji ambao wanao tafuta ukombozi kwa kupitia njia ya bahari. Barua inasema ni muhuimu kuzuia kupoteza maisha ya watu baharini lakini pia umuhimu wa kuwa makini kwa watu ambao wanaishi katika kambi hizo, ambapo serikali ya Austaralia inapaswa kuwajibika kutoa makazi mengine mapya kwa haraka.
Ni muda mrefu sasa ambapo kumekuwa na mjadala kimataifa unao husu ukiukwaji wa
haki za wahamiaji katika kambi la wakimbizi huko Manus ambapo wanasubiri kambi hiyo
ifungwe.Kwa namna hiyo Barua ya Askofu Nguyen inatoa ombi kwa serikali ya Austraia
kuheshimu wajibu wa Kimataifa, na kufanya kazi pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali
ili kuhakikisha usalama wa wale wanao tafuta hifadhi.
Ikumbukwe kuwa Canberra ilihukumiwa tayari kulipa Euro milioni 47 katika dola za Australia
kama fidia kwa ajili ya wanao tafuta ifadhi kati ya mwaka 2012 na 2014 huko Manus
ambao walilalamikia utaratibu mbaya.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |