Hivi karibuni umemalizika uzoefu wa Scholas Occurrentes huko Missao Mangunze nchini Musumbiji. Kwa wiki moja vijana kutoka katika shule mbalimbali za Jumuiya za Mangunze, Manjacaze, Chongoene e Xai Xai waliunganika pamoja kutafakari masuala yanayowahangaisha zaidi, hasa kama ya madawa ya kulevya, ukosefu wa usafiri kuwafikisha mashuleni, unyanyasaji wa kijinsia na utoro wa walimu. Wamesindikizwa na kikundi cha kimataifa cha Scholas na watu mahalia wa kujitolea walio andaliwa miezi ya hivi karibuni nchini Argentina.
wanafunzi hao waliwasilisha mapendekezo yao wakati wa hitimisho ya kazi ya Mkutano
wao mbele viongozi wa serikali mahalia wakiwepo Gavana, Alberto Zeca; , Msimamizi
wa wilaya Chongoene Carlos Buchili, Mkaguzi wa Elimu wa Wilaya Francisco Machava,
kamanda wa Polisi wa wilaya Chongoene José Ernesto Divis , Kiongozi mkuu wa eneo
hilo la Conceicao, Bw.Samuel Jose Chitambo na Paroko, Padre Juan Gabriel Arias.
Wanafunzi waliwaeleza vikwazo vikubwa wanavyokubana navyo kila siku; kwani wengi wao
wanalazimika kutembea kila siku kati ya km 5 na 10 kwenda tu na hivyo pia kurudi ili
kufika shuleni kwao kutoka katika vijiji na vitongoji vyao.Kutokana na hilo, wanafunzi
wanaomba usafiri wa kwenda na kurudi nyumbani kwao, wakati huohuo wameomba pia uboreshaji
wa njia za ufundishaji katika mafunzo ya walimu, bila kubaguliwa kwa upande wa wale
wanao kuwa wa mwisho, aidha uboreshaji wa miundo mbinu na vifaa.
Halikadhalika vijana wameonesha bayana uwepo wa vibanda haramu karibu na shuleni
kwao vinavyo uza madawa ya kulevya na pombe. Katika suala hili vijana wanatoa wito
uwepo wa mpango wa sheria inayo zuia ujenzi wa vibanda karibu na maeneo ya shule.
Kijana wa Umri wa miaka 17 kutoka katika Shule ya Sekondari ya Dambine 2000 ameeleze
kwa shahuku juu ya mkutano hu. Scholas ni sehemu muhimu ya mkutano kwa vijana , kwa
sababu ya kutoa fursa ya uwezekano wa kujadiliana matatizo yanayo wahangaisha katika
jumuiya zao, shuleni kwao na katika familia zao. Hii inatia moyo jinsi gani katika
maisha yao ya kila siku wanaweza kujikimu na kujiendeleza katika jumuiya zao kwa
kufanya kazi kwa pamoja kwa ajili ya kupinga na kudhibiti matatizo ya ulevi, madawa
ya kulevya vurugu na aina nyingine za matatizo.
Wakati wa kazi yao wamejikita zaidi vijana kutafuta ushauri kwa wataalamu na wawakilishi
wa jumuiya zao wali wasinidkiza katika wiki nzima. Kazi ya walimu na wataalamu hawa
imekuwa muhimu sana kutokana na lengo la kukuza program hizi katika malengo ya kuhamasisha
mikutano kati ya vijana lakini pia kuwapa sauti kwani watakuwa na fursa ya kutoa madai
yao na mapendikezo ya kuboresha ndani ya jamii zao pia mwendelezo wa umoja.
Walimu walikubaliana kuwa aina hii ya mikutano ya kuwaunganisha vijana ni msaada na
wenye thamani ya aina yake. Kwa njia hiyo unaweza kuhakiki kwa mara nyingine wito
na ujumbe wa ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko anaye weka wazi juu ya maendeleo
na mabadiliko ya hali halisi ya kijamii kwamnza yaanzie katika elimu. Timu ya Scholas
kimataifa kwa siku chache za hivi karibuni itaacha nchi ya Msumbiji , lakini itakuwa
imepanda mbegu ya matumaini kwa vijana 180 ambao wanaweza kubadili mtazamo wa jamii
husika.
Scholas Occurrentes ni Taasisi ya Kipapa yenye kuwa na lengo la kuhamasisha na kutetea, kwa njia ya elimu, sanaa na michezo, utamaduni wa kukutana kati ya vijana wa dini zote, ili kuchangia katika ujenzi wa jamii bora kupitia nguzo ya mazungumzo katika kuhakikisha amani duniani. Leo hii Scholas Occurrentes imeshasimika mizizi katika nchi 190 duniani kote, ikiwa na mtandao zaidi ya mashule 446,000 na mitandao ya kielimu kwa madhehebu yote ya dini, umma na binafsi. Tangu Juni 2017 imekuwa na makao yake makuu katika mji wa Vatican.
Sr Angela rwezaula
Idhaa ya kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |