Hivi karibuni huko Juba nchini Sudan ya Kusini wamefungua ofisi mpya za Caritas
Internationalsi, ofisi ambayo itaweza kusaidia dharura katika hali za kibinadamu.
Ni majengo mawili ya Caritasa ambayo yamefunguliwa na Askofu Mkuu wa Juba Paulino
Lukudu mjini Sudan ya Kusini.
Katika hotuba yake, akiwaelekea wahudumu wa Caritas mahalia, amewatia moyo katika
huduma yao wanayoitoa pia kuonesha umuhimu wa huduma yao kuwa ni kwa ajili ya nchi
yao na katika dunia. Kwa maneno hayo amewataka wafanye kazi kwa shahuku na juhudi
za kuboresha nchi; kwa kushirikiana na Kanisa ambalo amesema lina jukumu kubwa la
utoaji wa huduma ya idadi ya watu.
Ikumbukwe, mwaka huu tarehe 26 Februari, Baba Mtakatifu Francisko alipotembelea Kanisa la Kiangilikan mjini Roma alikuwa ameonesha hamu ya kutembelea nchi ya Sudan ya Kisini akiwa pamoja na Askofu wa Kianglikan Justin Welby. Lakini Safari hiyo haitafanyika mwaka 2017 kwasababu bado iko katika hoja , lakini wakati huo huo Papa hajasahau nchi hiyo ambayo tangu 2013 imeharibiwa na vita kati ya viongozi wa kisiasa. Kwa njia hiyo, mwezi wa Juni 2017, Kardinali Peter Turkson Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya huduma na maendeleo ya Binadamu aliwasilisha katika vyombo vya habari Mpango wa Baba Mtakatifu wa kusaidia Sudan ya Kisini hasa katika sekta ya Afya, elimu na shughuli za kilimo kwa kiasai cha jumla karibia nusu milioni ya dola za kimarekani ambazo Baba Mtakatifu Francisko ameamua kuonesha upendo wake na ukaribu wa taifa hilo la Sudan ya Kusini barani Afrika.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.
All the contents on this site are copyrighted ©. |