Katika Katekesi ya Baba Mtakatifu ya kila Jumatano mjini Vatican, hata leo tarehe 9 Agosti 2017 ameendelea na Katekesi yake katika Ukumbi wa Mwenye Heri Paulo VI. Katekesi yake imegusia kuhusu msamaha wa Mungu ni kama injini ya matumaini.Tafakari yake imetokana na Injili ya Mtakatifu Luka kuhusu mwanamke aliye mnawisha miguu Yesu kwenye nyumba ya Simon aliyokuwa amekaribishwa, hivyo ndipo Yesu “akamgeukia yule mwanamke na kumwambia Simoni, “Unamwona huyu mwanamke, sivyo?. Basi, mimi nilipoingia hapa nyumbani kwako hukunipa maji ya kunawa miguu yangu; lakini mwanamke huyu ameniosha miguu yangu kwa machozi yake na kunipangusa kwa nywele zake. Kwa hiyo nakwambia amesamehewa dhambi zake nyingi kwa kuwa ameonyesha upendo mkubwa. Mwenye kusamehe kidogo, hupenda kidogo.”basi, Yesu akamwambia yule mwanamke, “umesamehewa dhambi zako.” Na hapo wale waliokuwa pamoja naye mezani wakaulizana, “Ni mtu wa namna gani huyu awezaye kusamehe dhambi?” Naye Yesu akamwambia yule mwanamke, “Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani.”
Baba Mtakatifu Francisko ameanza akisema kuwa wamemsikiliza Mfarisayo Simoni akisema ni nani huyo anaye samehe dhambi (Lk 7,49). Hiyo nikutokana na kwamba Yesu amemamaliza kutenda jambola aibu . Kwani Mwamke huyo katika mji alijulikana mwenye dambi na akaingia masikini akiwa amejificha katika nyumba ya Simoni, alitaka asijulikane ili asije akauwawa kama ilivyokuwa kasumba ya wakati huo. Aliinamia miguu ya Yesu una kunawisha na baadaye akampaka mafuta ya kunukia. Wote ndani walianza kunung’unika wakisema Kama Yesu angekuwa ni Nabii asingekubali kufanyiwa ishara ya namna hii ya mwanamke kama huyo. Katika mantiki ya wakati Baba Mtakatifu Francisko anafafanua, kati ya mtakatifu , mwenye dhambi , kati ya msafi na mchafu , ubaguzi ulikuwa lazima ufanyike kwa hakika.
Lakini kwa mantiki ya Yesu mtazamo wake ulikuwa tofauti. Tangu mwanzo wa utume
wake huko Galilaya, yeye aliwakaribia wakoma, wanye mapepo wabaya, wagonjwa na waliobaguliwa.
Tabia ya namna hiyo haikuwa ya kawaida, kwani tabia ya Yesu mbele ya uchungu huo uliamsha
hisia ya moyo wake wenye upendo mkuu kuwakaribia na kuwapenda watu walio baguliwa
na wasioguswa ambapo baadaye ukaleta mafarakano kati ya watu wake.
Pale ambapo kuna mateso, ndipo Yesu anakuwapo,hubeba hayo matatizo, na mateso hayo
yanakuwa ya kwake anasema Baba Mtakatifu.Yesu hakuhubiri kwamba hali ya mateso inapaswa
kuvumiliwa kwa ujasiri, kama vile ya wataalamu wa filosofia ya wakati ule. Yesu anashiriki
mateso ya binadamu anapokumbana nayo ndani ya moyo wake na ndiyo tabia ya kikristo:
katika huruma,Yesu anafanya uzoefu wa mateso.Kwa maana nyingine Yesu anasikia mateso
ndani ya mwiliwa wake. Ni mara ngapi katika Injili tunakutana hali ya namna hiyo.
Moyo wa Yesu unatwaa na kuonesha moyo wa Mungu , mahali ambapo kuna binadamu, mke
na mme anayeteseka na kutaka kuponywa, kukombolewa mateso yake.
Kwa njia hiyo Yesu anafungua mikono yake kwa ajili ya wadhambi. Ni watu wangapi
waddhambi hata leo wanaendelea katika maisha yaliyokosewa , na hawana mtu wa kuwa
tayari kuwatazama au kuwatazama kwa namna tofauti yaani , kwa macho yenye huruma,
au kusema zaidi kwa moyo wa Mungu maana yake kwa matumaini. Yesu mwenyee anaona
huo uwezekano wa kufufuka hata katika uchanguzi mwingi wa makosa au kuosea njia.
Baba Mtakatifu ameonesha akisema, mara nyingi ipo hali ya kusahau kwamba ,Yesu aliingia
katika upendo usio rahisi, na usiyo kuwa na faida. Injili zinaonesha, matukio hasi
juu ya Yesu na hasa pale anapo samehe dhambi kwa mfano wa mwanaume aliyekuwa amepooza
(Mk 2,1-12). Ni mwanaume aliyekuwa anateseka mara mbili kwasababu alikuwa hawezi
kusimama na alikuwa anajisikia mwenye dhambi. Yesu alitambua uchungu wake jinsi ulivyo
kuwa mkubwa na ndiyo maana alimkaribisha na kumponya akisema mwanangu umesamehewa
dhambi zako. Baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wameketi hapo wakawaza mioyoni mwao
kuwa amekufuru, kwasababu hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke
yake .
Anasisitiza Baba Mtakatifu akisema, sisi tuliozoea kufanya uzoefu wa msamaha wa dhambi, labda hata kuzidi kiasi, tunapaswa wakat mwingine kukumbuka jinsi gani upendo wa Mungu ulivyonunuliwa kwa gharam kubwa. Yesu hakubambwa msalabani kwasababu ya wagonjwa kupona, kwasababu ya kuhubiri upendo au kwasababu ya kutangaza heri . Mwana wa Mungu anatundikwa msalabani kwasababu amesamehe dhambi, kwasababu anataka uhuru wa kamili wa moyo wa binadamu.Yesu hakubali kwamba binadamu amalizie maisha yake yote akiwa na chale isiyofutika katika mawazo ya kutokuweza kupokea ndani ya moyo wake ile huruma ya Mungu. Kwa njia hiyo wadhambi wanasamehewa, na siyo tu kutulizwa kwa tabia za kisaikolija , kama sababu ya kuwa huru kwa mantiki ya dhambi. Yesu anafanya zaidi ya limu ya saikolojia maana anatoa fursa ya mtu aliye kosea kuwa na matumaini, pia kuwa kiumbe kipya, yaani maisha yanayojikita ndani ya upendo. Matayo mtoza ushuru aligeuka kawa mtume wa Kristo. Zakayo mtoza ushuru na tajiri huko Yeriko alibadilika akawa mfadhiri wa masikini, Mwanamke msamaria aliyeolewa na wanaume watano,wakati huo alikuwa akiishi na mwingine asiye wa kwake,aliahidiwa chemichemi ya maji ya uhai wenye maisha ya milele (Gv 4,14).
Baba Mtakatifu Francisko amemalizia katekesi yake akisema ni vizuri kufikiria kwamba Mungu hakuchagua kufinyanga na kutengeneza Kanisa na kuliweka juu ya watu wasio kosea kamwe. Kanisa ni watu wadhambi ambao lakini wanafanya uzoefu wa huruma na msamaha wa Mungu . Petro alitambua ukweli mwenyewe baada ya jogoo kuwika. Pamoja na ukarimu wake na mambo mengi yaliyokuwa yakimvimbisha kifua kwa kujisikia yeye kuwa zaidi ya watu wengine. Wote ni tu masikini wadhambi ni wahitaji wa huruma ya Mungu mwenye kuw na nguvu ya kutubadili, na kutupatia matumaini kila siku. Watu waliotambua ukweli huo msingi Mungu anawapatia utume mzuri duniani. Kwa maana ya kusema upendo kwa ndugu kaka na dada, na kutangaza huruma ya kwamba Mungu hamkani hata mmoja. Na hiyo ndiyo matumani, hivyo basi tuendelee mbele na matumaini hayo ya msamaha, katika upendo na huruma ya Yesu.
Mara baada ya katekesi yake kama kawaida amewasalimia mahujaji wote walio fika katika ukumbi , wakati huo huo na vijana akisema wanaotembelea katika sehemu za utamadnui kama vile sanaa, na kwamba iwe kwao fursa ya kutambua na kufuata nyayo kwa mifanoiliyo achwa na mashuhuda wengi wa Injili kama vile Mtakatifu Laurent ambaye tarehe 10 Agosti kanisa linamkubuka. Anawatia moyo wagonjwa wote waungane kila wakati na mateso ya Yesu wakibeba msalaba kwa imani ya ukombozi wa dunia. Aidha wenye ndoa wapya ambao hawakosi kila wakati katika katekesi yake Baba Mtakatifu amewatakia familia zao mpya ziwe na imani ya Injili na katika upendo.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili
All the contents on this site are copyrighted ©. |