2017-08-08 16:52:00

Askofu Mkuu Kaigama nchini Nigeria amesikitishwa na shambulizi


Inasemekana waathirika 11 na majeruhi wasio kuwa na idadi katokana na shambulizi la Kanisa la Mtakatifu Filippo huko Ozubulu Kusini  Mashariki mwa Nigeria Jumapili asubuhi ya tarehe 6 Agosti 2017. Kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari mahalia na  Polisi wanasema mtu mmoja aliingia Kanisani wakati watu wanasali na kuanza kushambulia  kwa kuwapiga risasi hovyo. Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Jose  na amabaye ni Rais wa Baraza la Maaskofu nchini Nigeria Ignatius Kaigama , ameelezea masikitiko yake akiwa nchini Italia. Anasema, ametafuta namna ya kuwasiliana na Maaskofu mahalia ili kupata habari kamili juu ya tukio hilo mara baada ya kupokea habari hizo.

Katika maelezo yake anasema hawajuhi sababu ya vitendo hivyo visivyo vya kibinadamu; aidha, siyo rahisi kabisa kufikiria kitendo cha namna hiyo dhidi ya watu wasio kuwa na hatia wakiwa  Kanisani  saa kumi mbili za alfajiri wakisali. Kwa mujibu wa uchunguzi, inasemekana sababu za tukio hilo likawa wahusiaka ni makabila kulipiza visasi na wala siyo tendo la kigaidi. Hii ni kutokana na kwamba eneo la mashambulizi yaliyotokea siyo eneo la kutishwa na kukundi cha kiislam wa  Boko Haram, ambao wamekwisha fanya mashambulizi kadhaa dhidi ya wakristo na hata waislam katika maeneo ya Kaskazini mashariki ya nchi hiyo. Jimbo la Nnewi ambalo ndimo Parokia ya  Ozubulu iko Katika Serikali ya Kusini mwa Nigeria mahali ambapo wakristo ndiyo walio wengi.

Askofu Mkuu Kaigama  ameeleza kuwa eneo hilo limejaa wakristo kwa wingi kwa maana ya kwamba ukatoliki katika eneo hilo umesimika mizizi kwa muda mrefu. Wamisionari wa kwanza walifika eneo hilo mwaka 1885. Kutokana na uzoefu wake ni kwamba  eneo hilo linaweza kuonekana matukio ya vurugu za kijamii, hasa zinazohusiana na ardhi katika masuala ya kilimo, lakini mashambulizi ndani ya Kanisa limekuwa ni tukio lisilotarajiwa kabisa.
Kwa njia hiyo Askofu Mkuu Kaigama anaomba, tukio hili la kigaidi liwe la kipekee na lisihusishwe na ugaidi, kwani anaongeza;Nigeria wamepata matatizo mengine na hawataki tena mivutano hiyo ikue. Wanahitaji amani kwasababu nchi yao ni yenye rasilimali nyingi ambazo zikitumika vizuri zitawaruhusu kuishi kwa amani.

Sr Angela Rwezaula 
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.