2017-08-05 15:57:00

Serikali nchini Malawi wapongeza vyombo Katoliki vya Habari!


Taarifa kutoka katika Shirika la habari Katoliki la CAN linasema, Waziri wa mawasiliano na tekenolojia  amepongeza vyombo  Katoliki vya Habari katika nchi mapema wiki hii kwa jitihada zao za uinjilishaji ikiwa ni pamoja na kuadhimisha siku ya 51 ya Mawasiliano duniani. Waziri wa habari Nicholas Daus amesema mkatoliki anaongeza msaada kwa Kanisa. Ameyasema hayo baada ya kutembelea ofisi ya Radio FM Tuntufye katika  kituo kilichopo Jimboni Karonga. Vilevile akizungumza na vyombo vya habari Katoliki katika Parokia ya Mtakatifu Maria huko Karonga amewahimiza wasikatishwe tamaa na upungufu wa masafa katika huduma yao. Aidha wawe makini,wasifurahishwe hata kidogo  habari mbaya au kitu ambacho kinaweza kuwadhuru wengine. Amesema kwa kutumia chombo cha habari cha  Kanisa ni muhimu kuendesha utume wa uinjilishaji. Amewasifu vikundi  vya wanahabari na kuthibitisha juu ya utoaji wa msaada wa serikali, na kwamba anavutiwa jinsi gani Tuntufye FM katika Jimbo la Karonga inavyofanya kazi vizuri.

Naye  Askofu Martin Mtumbuka wa Jimbo la  Karonga nchini Malawi  wakati wa kuadhimisha Misa Takatifu katika mahubiri yake  amesema mambo yote mawili yanatoa changamoto na akatoa shukrani kwa wale wote waliokusanyika. Pamoja na hayo amechangamotisha nyumba za vyombo vya habari zao na wale wanaofanya kazi katika vyombo hivyo kwamba angependelea vyombo hivyo viwe vya kitaalam na pia wafanyakazi wawe wataalamu zaidi. Hata hivyo amemshukuru Mungu kwa zawadi ya vyombo vyote vya mawasiliano, pamoja na kwamba amesema, changamoto  ni kwao binafsi ya kuweza kuzitumia  kwa ufanisi. Ameongeza kusema  inawezekana kufanya vizuri zaidi kuliko kile kinachofanyika katika vituo vya televisheni, redio na magazeti. 

Askofu aliongeza kusema,"Hebu tutoe ujumbe wa imani kwa ajili ya utukufu wa Mungu na maendeleo ya taifa hili”.Sisi ndiyo wanaopigania hii, hii inaweza kufanyika kulingana na msingi  wa jinsi gani tunavyofanya mambo. Hebu tufanye mambo kwa njia ya kuratibu na kuwa na ubunifu”Amesema.
Katika maadhimisho hayo  pia Askofu George Tambala wa Zomba ambaye ni Rais wa mawasiliano wa Baraza la maaskofu nchini Malawi, alitafakari kuhusu ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko wa Siku ya Mawasiliano ya 51 Duniani  akisema,  Baba Mtakatifu Francisko  anatuhimiza sote kuvunjavunja mduara wa wasiwasi na kuongeza hofu ambayo husababishwa kukazia mara kwa mara habari mbaya kama vile vita, ugaidi, kashfa na kila aina ya kushindwa kwa binadamu.

Aidha  amebainisha kuwa ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko unachangamotisha kwamba waandishi wote wa vyombo vya habari wanapaswa kutafuta njia ya wazi,ya ubunifu ya mawasiliano ambayo haitukuzi uovu lakini badala yake ni kuzingatia ufumbuzi na kuhamasisha njia nzuri na pendelevu kwa upande wa mpokeaji wa habari hiyo. Vyombo vya habari Katoliki nchini Malawi vinajumuisha tume ya Maaskofu  ya mawasiliano ya kijamii kama vile Radio Maria Malawi; Radio Alinafe; Tigabane ; Tuntufye FM; Televisheni ya Luntha, Montfort na Gazeti la Likuni.

Sr Angela Rwezaula 
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.