Ubinadamu mkubwa ambao nchi inataka kujaribu kufanya ni kupokea wakimbizi , historia nyingi za amani mapatano ambazo viongozi wa kikristo na waislam wanajaribu kwa njia zote kutekeleza. Haya ni mambo muhimu makuuu ambayo yameshangaza sana Askofu Mkuu wa Canterbury Justin Welby ambaye ni kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya kianglikan nchini Uingereza ,ambaye yuko katika matembezi kwenye nchi ya Sudan, na siku hizii yuko katika Jimbo la Kadugli kwenye milima ya Nuba, mahali ambapo alikutana na viongozi wa madhehebu ya kidini pia namba kubwa ya wakimbizi ambao amepata kuwasikiliza na kuongea nao.
Katika maadishi yake Askofu Mkuu Welby kwenye ukurasa wa mitandao ya kijamii
wa Facebook anasema
kuwa ni fursa yake ya pekee kuitembelea nchi ya Sudan . Mambo mawili yamemshangaza,
hawali ya yote ni jinsi gani nchi hiyo wanakabiliana na wakimbizi wengi hivyo. Nchi
ya Sudan ni mfano wa kuigwa na watu wengi katika dunia hii kwa ajili ya wakimbizi
na wenye kuhitaji. Anaongeza kusema kuwa anaamini kwamba, kupokea wakimbizi wengi
namna hii imekuwa ni changamoto kubwa na watu wa Sudan wameonesha kuwa na ubinadamu
wa kweli.
Jambo la pili ambalo limestahajabisha Askofu Mkuu Welby ni matumaini ya watu wa Sudan waliyo nayo kwa ajili ya amani na mshikamano na ambao nchi leo hii inatarajia. Anayasema hayo kutokana na kusikiliza na kuongea na viongozi wa kikrsto na kiislam huko Madugli, na kwamba amesikia historia za watu wote wanao taka amani, ambao wako bega kwa bega wakitafuta namna ya kufikia amani hiyo ya kweli. "Nchi ya Sudan kweli inahitaji amani kwa maana inatambua zaidi ya wengine gharama ya vita ni nini". Kwa njia hiyo Askofu Mkuu Welby anawaalika waamini wote kusali ili ulimwengu mzima uweze kuheshimu na kufanya hadi ya kuweza kuisaidia Sudan ya Kusini.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |