2017-08-01 14:13:00

Hacheni kujipendelea binafsi bila kufikiria nchi na vizazi vijavyo


Wachimbaji haramu madini ni raia waovu ambao wanatishia na kuharibu nchi kwa kujiwekea maslahi yao binafsi kwa ujumla. Hayo ni maneno ya kukemea kutoka kwa  Askofu Mkuu Gabriel Justice Yaw Anokye  wa Jimbo kuu la Kumasi nchini Ghana.
Mtukio haya yajulikanayo  galamsey,ni wachimbaji haramu wa madini ya dhahabu , wamekuwa tishio linalokithiri nchini Ghana kwa namna ya pekee katika mito na hifadhi ya maji ya taifa, ambayo yamechafuka kwasababu ya mchanganyiko wa kutumia zebaki katika kudondoa dhahabu kutoka katika miamba inayotoa dhahabu hiyo. Askofu amesema  katika kujifikiria tu wao wenyewe bila kuzingatia taifa maana yake ni kuwa na tamaa na maovu na hivyo inalazimu  kila mmoja  kufikiria kuhusu mstakabali wa nchi na vizazi vijavyo.

Kwa upande wa Askofu Mkuu  anafikiria kwamba wachimbaji haramu ni zaidi wa watu waovu na pia watu wa hatari  na wauaji wa wauaji wa watu bila huruma. Ni watu wasio fikiria nchi yao na watu wake.Pamoja na kwamba serikali ilianzisha kampeni ya kuzuia shughulia hizo haramu za galamsey, lakini Askofu anatoa taarifa kwamba watu hawa wanaendelea na shughuli hizo wakati wa usiku katika maeneo kama vile ya Tmso, Modaso na Diaso. Nchi ya Ghana ni ya pili katika uzalishaji wa wa dhahabu barani Afrika na ni  nchi ya Kumi duniani. Pamoja na migodi ya kisheria iliyopo, lakini istoshe bado ipo nyingine ya kisirisiri. Ni vigumu kuwahesabu makundi haramu ya Galamsey ; inakadiriwa kati ya 30,000 hadi 200,000 ya watu na badhi yao ni wageni  hata kutoka nchi ya China. Kumasi ni mji mkuu wa mkoa wa Ashanti ya Kusini mwa Ghana ambapo akiba ya dhahabu yote ya nchi inapatikana.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.