2017-05-21 10:52:00

Kard.Filoni:Maaskofu wanapaswa kuwa wachungaji na Baba wa waamini


Kardinali Fernando Filoni, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa watu, ambaye tangu tarehe 18 hadi 25 Mei 2017 atakuwa  katika  hija ya kitume nchini Equatorial Guinea  Jumamosi  tarehe 20 Mei 2017 ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu na kuwaweka wakfu Maaskofu watatu wapya walioteleuliwa hivi karibuni na Baba Mtakatifu Francisko.
Katika mahubiri yake amesema Baba Mtakatifu Francisko mtume wa Khalifa Petro mtume wa Yesu amepata uwezo wa kuwaimarisha ndugu kwa ishara ya kibaba juu ya watu wa Equatorial Guinea , kwa njia ya peke ya kufikiria jumuiya ya wanakatoliki wapendwa wa nchi hii. Tarehe 1 Aprili 2017 walitoa uamuzi wa kuunda majimbo mapya ya Mongono na Evinayong, na kuteua askofu mchungaji mwingine kwa ajili ya jimbo lililobaki wazi la Ebebiyin.Na kumteua Askofu mpya mteule Juan Domingo-Beka Esono Ayang  wa Jimbo Katoliki Mongomo.  Askofu jimbo jipya  mteule Calixto Paulino Esono Ebaga Obono, Askofu wa kwanza wa Jimbo jipya  Katoliki la Evinayong. Askofu mteule Miguel Angel Nguema Bee, amewekwa wakfu kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Ebebiyin.

Kardinali Filoni anaendelea, hawa na watoto watatu wa nchi hii ambapo Bwana Yesu kwa njia ya liturujia ya daraja la kutoa wakfu wa kiaskofu wanapewa zawadi ya Roho Mtakatifu katika ujazo wa kikuhani. Wao wameitwa kwa ajili ya kutoa huduma ya Mungu na huduma ya jumuiya ya kikristo kama makuhani. Leo hii wanaalikwa kujikita katuka Kanisa kama Baba na wachungaji wa watu wa Mungu ambao wamekabidhiwa , watu walio kombolewa na kutakatifuzwa na Kristo kwa njia ya sadaka msalabani.Kama tunavyotambua nchi ya hii inashi kipindi muhimu cha kihistoria katika kuachanua kwa uinjilishaji. Kwa njia ya kuimarisha utume wa kimisionari ambao ulianzishwa wakati uliopita na wamisionari  wa nyakati zile ambao walijitoa maisha yao kwa ajili kueneza Injili na maskini , uamuzi huu wa Baba Mtakatifu  ni kutaka kundeleza mchakato mzima kwa ndani ya nchi  ambao ni kwa ajili ya maendeleo ya Kanisa katika nchi hii.

Kipindi hicho cha kihistoria , kinawakilisha utambuzi wa safari ya ukomavu wa historia ya sasa  licha ya matatizo mengi ya wakati ulio pita. Kwa njia hiyo Kardinali Filoni anapendelea kutoa pangezi kushiriki kati yao siku njema ya kipekee akimwakilisha Baba Mtakatifu aliyemtuma kuwatia moyo waamni na watu wote wa chi.Kwa namna hiyo amesema anatoa salam kwa Rais wa nchi hiyo na  watu wake wote.
Lituturujia ya neno la Mungu lilongoz maadhimisho yao  limetaka kukumbusha kwamba tunacho kitenda leo hii siyo tofauti na maisha ya wakristo wa kwanza miaka 2000 iliyopita. Kwa dhati baada ya kupaa kwa Bwana mitume walitambua kwamba katika Kanda ya Samaria walikuwa wamepokea Neno la Mungu na wakaamua kumtuma Petro na Yohane, ili mwisho waweze kutambua jinsi gani watu wa Samaria walikuwa na imani. Katika mji wa Samaria yaliishi makundi ya ambayo hayakuwa ni ya kiyahudi, lakini ambao walina kuundwa kwa jumuiya ya wafuasi wa Yesu na hivyo ilikuwa muhimu wa uwepo wa utume  ili kuweza kugundua na kuwahimarisha waamini wake imani.

Kwa maana hiyo katika nchi hii ya Guinea, Neno la Mungu lilipandwa na wamisionari kwa miongo mingi iliyopita , ambao waliunda jumuiya za kwanza za kikriso na pia vikawepo vituo vya kwanza vya kimisionari na maparokia ya kwanza , na mwisho kuundwa  kwa majimbo, ambayo yaliongeza kutoa matunda ya Kanisa la Gunea : Yote hayo yaliwezekana kwa neema ya Neno la Mungu kutangazwa na kupokelewa na mababu zenu .
Halikadhalika amesema;  utume huo unaendelea  na kfanya kwamba Baba Mtakatifu anawapatia maaskofu wapya watatatu wanao wekwa wakfu. Wao watakuwa na jukumu kama hilo la Petro ana Yohane , wa kuimarisha na kukuza mbegu ya Neno la Mungu . Wao watakuwa kwenu  kama Baba na wachungaji. Hiyo  ni kwasababu Balozi wa wa Kitume wa Vatican wakati wa mchakato wa kutafuta maaskofu wapya alipowauliza waamini kutaka kujua ni askofu gani wanayemtaka  wengi waliandika kwamba wawe watu wa Mungu, wa sala, baba  na kuwa wachungaji na siyo tu kuwa viongozi.

Kardinali Filioni akiwageukia maakofu walioitwa katika daraja wa kiaskofu:  hawali ya yote wanapaswa kuwa watu wajasiri, thabiti katika kutoa ushuhuda wa imani , na kwa njia hiyo wawe wahamasishaji wa huduma ya uinjilishaji na wahudumu wa watu wa Mungu ambao wamekabidhiwa. Wao ndiyo wako mstari wa mbele katika kuwajibika kwanza katika utume na kwa njia yao wanaungana na mapadre, watawa na walei wote kwa ukarimu katika utashi wa kishirikiana nao. Anawashurukuru kwa ajili ya kukubali kwa ukarimu utume huo  mgumu wa shughuli ya Kanisa.
Kardinali Filoni anaongeza kuwaeleza kwamba, wao siyo viongozi wa kabila au wa serikalii , bali ni  wachungaji daima wa wote. Wito wa kuwa askofu daima ni ule unaokufanya kuwa  tayari  kufanya mapenzi ya Bwana. Kwa njia hiyo kuna uraha na mateso.Lakini kama vile katika familia yenye , baba, mama na watoto, hapakosekani kipindi cha furaha na mateso, na hivyo hata wao mambo hayo hayatakosekana.

La muhimu ni kutambua katika upeo wa kikriso yote ni zawadi na neema kwa Mungu . Sisi hatuwezi kamwe kusema tunasatahili mbele ya mengi tunayopokea kutoka kwa Bwana. Hiyo ni dhahiri kwasaba bni yeye kwanza anayetuita  na pia kujua mahali gani anatutuma katika utume wa kuendela kutangaza Injili na kusaidia kuimarisha  Kanisa.
Bwana amewachagua siyo kwa ajili ya mastahili yenu labda zaidi ni kwa ajili ya mapuungu yenu, na kwa njia hiyo asiwepo hata mmoja wenu kujidai. Kumbukeni maneno ya mtume Petrombele ya Yesu aliyekuwa anataka kumkabidhi zizi lake aliongoze , alitamka kwa unyenyekevu kwamba nenda mbali na mimi Bana maana mimi ni madhambi , lakini wajua ni jinsi ani ninakupenda , wajua udhaifu wangu.Hata hivyo Bwana aliweza kumwimarisha na kumkabidhi Kanisa lake.

Mwisho amesema kwa wote wote wambaao yenye sura ya kanisa Kuu moja na majimbo manne nchini Guine  kwamba wanapaswa kusaidia kujenga kwa kina umoja kwa ajili ya wema wa watu wote wa nchi. Uwepo wa majimbo mawili mapya , maaskofu wanateza kuwa karibu na watu na kwa njia hiyo Kardinali Filoni anamatuamani ya kwamaba wanateza kuwafikia .Kwababu haya majimbo yameundwa kwa ajili ya  kutaka kuwasaidia ninyi. Lakini kumbukeni  kwamba majengo tu hayatoshi iwapo utakosekana ushirikiano. Jambo muhimu ni kuimarisha uwepo wenu na kuwa sehemu ya Kanisa katika ulimwengu , kama vile katika majimbo yenu mahalia kushirikiana katika maisha ya jumuiya na kuyafanya yakue.

Kwa namna ya pekee majimbo mapya ya Mongomo na Evinayong, ni kama karatasi nyeupe isiyokuwa na maandishi kwa ajili ya kuandika katika kitabu kikubwa cha Kanisa. Ni nyinyi manaopaswa kuandika historia ya maisha ya kila mmoja , kwa kushirikishana na kuifanya ikue kwa furaha na ukarimu.
Ndugu wapenda upendo ni nguvu na kujenga  na kukuza, kwa njia hiyo penda Kanisa lenu na kulisaidia zaidi badala ya  kulichambua na kubainisha makosa. Ni kwa njia ya kupenda na kushirikiana mnaweza kiimarisha na kufanya ukue utume wa kuinjililisha. Maendeleo endelevu ya maadili ya Kanisa la Guine iko mikononi mwenu, Maskofu wenu ni wazalendo kama ilivyo  mapadre wenu, na watawa wenu. Uamuzi uko mikononi mwenu !

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.