2017-05-18 17:20:00

Tani milioni 90 za Vyakula zinatupwa Ulaya wakati wengine wanakufa na njaa


Kila mwaka Ulaya karibu tani milioni 90 za ya vyakula zinatupwa kwenye jalala. Ni matumizi mabaya yanayohusisha hata familia: kila mzalendo anatupa chakula kwenye takataka karibu kilo mbili kila siku ambazo bado zinangeweza kutumika kwa wiki. Ni takwimu za kutisha kabisa   za kutokuweza kuvumilai ukifikiria kwamba katika maeneo mengi ya sayari hii watu wengi wanakufa kwa  njaa. Kwa njia hiyo, Kamati ya Shirikisho la Baraza la Maaskofu Ulaya (Comece ) wametafuta ufumbuzi wa pamoja mapema wiki hii katika Bunge la Ulaya, wakitoa wito wa  nchi wanachama wa Ulaya kupunguza matumizi mabaya ya chakula.

Katika Gazeti  Osservatore Romano linaandika , Bunge la Ulaya huko Bruxelles , wamesema kupunguza matumizi mabaya ya vyakula kwa asilimia 30% kufikia mwaka 2025 , na asilimia 50 kufikia mwaka 2050 kulingianishwa na mwaka 2014.
Kati ya maombi mengine yaliyotolewa ni kutafuta ufumbuzi wa kutokuwa na vizingiti vya kusaini na mbunge wa Croatia Biljana Borzan, ambaye ametoa kodi  ya kutoa chakula  inayohusiha Kanisa la Ulaya na pia viongozi wa kila mwanachama wa Ulaya, ili waweze kuwa wazi kwenye tiketi zinazoonesha muda wa matumizi ya chakula kinachotolewa na mwisho wa matumizi yake.

Katika ujumbe uliotolewa katika mtandao wa Kanisa, Padre Olivier Poquillon wa Shirika la Kidomenikani , ambaye ni katibu Mkuu wa Shirikisho la Baraza la Maaskofu wa Ulaya anabainisha kuridhika na jinsi walivyotafuta ufumbuzi muhimu ambao ni mwongozo wa Baba Mtakatifu Francisko, ambao mara nyingi amesisitiza bila kuchoka akipinga utamaduni wa kubagua, ambao daima unawaacha waathirika kutokana  na matumizi mabaya ya vyakula. Ni mada ambayo Baba Mtakatifu alikumbusha katika hotuba yake kwenye Bunge la Ulaya tarehe 25 Novemba 2014 , akisema, haiwezekani kuacha mamilioni ya watu wanakufa duniani kwa ajili ya njaa wakati tani za vyakula vinaendelea kutupwa kila siku katika meza zetu.
Kwa mantiki hii Katibu Mkuu wa (Comece) anabainisha kwamba kura za Bunge la Ulaya zinapaswa kutafakari kwa kina  na kamati ya Ulaya kama Ishara ya kutia moyo , ili kuweza kuharakisha sheria ya dhati ya  Baraza la Ulaya kujikita katika matendo kwa ujasiri, kuwawezesha watu na hasa wadahu wake kwa namana ya pekee watumiaji ili kuondoa ile kashfa ya matumizi mabaya ya kutupa vyakula.

Shirikisho la Baraza la Maaskofu Ulaya (Comece), linatatarajiwa mawazo ya malengo hayo kutotiliwa vizingiti maana yanakwenda sambamba na malengo ya melendeleo endelevu ya Umoja wa mataifa. Hiyo ina maana kwamba Tume ya Ulaya lazima kuimarisha kazi yake; kwa mtazamo huo, kazi muhimu zaidi ni kuwafanya wanaulaya wawe na  ufahamu wa madhara ya kijamii ya kutupa chakula ambacho bado kinaweza kutumika . Hivyo Parokia na harakati za vyama vya Kikanisa ni lazima kuhakikisha kutoa machango wao wa kuhamasisha zaidi jamii.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.