Kardinali Angelo Amato , Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya kuwatangaza watakatifu,
amefanya mahojiano ya Mwandishi wa Radio Vatican, kuelezea maisha ya Louis Antoine
Ormières ambaye atatangazwa mwenyeheri huko Oviedo Hispania tarehe 22 Aprile 2017.
Louis Antoine Ormières alizaliwa tarehe 14 Julai 1809 huko Quillan mji mmoja kusini
mwa Ufaransa, unaopakana na nchi ya Hispania. Alipata daraja la upadre mwaka 1833
, na kujikita katika shughuli za kitume kwa ngazi ya elimu na kufundisha vijana.
Mwaka 1839 akaanzisha Shirika la kike kwa jina la Malaika Walinzi, ambapo jina linejieleza
karama ya shirika hilo. Alikufa katika hali ya utakatifu tarehe 16 Januari 1890 baada
ya kuwa ameanzisha mashule 87 huko Ufaransa na Hispania.
Kuhusiana na utakatifu wake, Mwenye heri alikuwa mwelewa na mwalimu wa kuzaliwa
, alikuwa amejaa karama za kikristo, imani , matumaini na upendo. Alikuwa amejaa ubinadamu
wa huruma na shukrani, vilevile mtulivu na rafiki. Kutokana na kuwa na huruma ya Mungu
ilimfanya kuwapenda walio wadogo, wadhaifu , masikini, na wasio kuwa na hatia. Yeye
alikuwa anaishi maisha na kufuata mafundisho ya Mtakatifu Paulo akisema “ Basi, kwa
kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu
wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu. (Wakol 3,11-12)
Aidha Kardinali Amato ameelezea baadhi ya mifano halisi ya matendo ya upendo aliyofanya
kuonesha kuwa ni mtakatifu kweli kwani amesema, zipo shuhuda nyingi zinaonesha upendo
wake kwa mfano wa kutetea mwanaume mmoja aliyekuwa ameonewa bia hatia, Alikuwa akitoa
makaribisho kwa wakimbizi kutoka Hispania, alimwombea kijana aliyekuwa anapaswa kutunza
familia yake mara baada ya baba yake kufa msaada kutoka kwa watu watajiri wamsaidie.
Alijikita kumtafutia msaada masikini mama mmoja na watoto wake wawili .Alimtia moyo
wa kibaba mtawa mmoja aliyekuwa mgonjwa sana.
Kwa mambo haya kadhaa na mengine yanaonesha kuwa alikuwa mtu wa Mungu na mtakatifu
kweli. Hata katika kitabu cha maisha yake , kinaeleza hali halisi zaidi . Alikuwa
ni mkarimu, kuwasaidia wagonjwa ambapo Askofu wake alimwita kuwa ni shahidi wa upendo.
Alikuwa akiwaalika watoto wake kiroho waige mfano wake na kuwasaidia wengine kufanya
hiyo safari ya kuiga. Alikuwa akiwambia kwamba watoto mnapaswa kuweka mabawa na kuwa
jasiri.
Amemalizia kwa kusema ni kwanini atangazwe kuwa mwenye heri,na kusema, karama ni
pete ya mkofu wa dhahabu ya utakatifu. Anaye bahatika kuwa nayo anapata hata nyingine
zaidi. Kwa njia hiyo ni dhahiri kutokana na imani kubwa aliyokuwa kuwa nayo , mifano
yake, tabia yake ya uvumilivu, upole , na unyenyekevu. Tunatambua ya kwamba unyenyekevu
ndiyo msingi wa kila karama, kwa njia hiyo Padre Ormières alikuwa na unyenyekevu
wa aina yake.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |