2017-03-10 11:13:00

Sala ya Jubilei ya Miaka 150 ya Ukristo, Tanzania Bara


Ee Mungu Mwenyezi/ Baba wa milele /tunakushukuru kwa zawadi ya Mwanao mpendwa Yesu Kristo /aliyetwaa mwili kwa uwezo wa Roho Mtakatifu / akazaliwa na Bikira Maria. / Yeye alihubiri neno lako/ na kukamilisha ukombozi kwa mateso / kifo na ufufuko wake wa ajabu./Hatimaye aliwaagiza Mitume wake akisema / “Enendeni ulimwenguni mwote mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. / Aaminiye na kubatizwa ataokoka / asiyeamini atahukumiwa/ (Mk 16:15-16).

Kwa kuitika agizo hilo/ wakati ulipowadia / kwa mapenzi yako uliwavuvia Watawa mashuhuri wa Shirika la RohoMtakatifu / ambao kwa ujasiri wa ajabu walifika huku kwetu/ wakausimika Msalaba katika kituo cha Bagamoyo./ Msalaba huo ni ishara ya ushindi wa Mwanao dhidi ya dhambi na mauti. / Wamisionari hao wakishirikiana na wenzao waliofika baadaye / walikuhubiri Wewe. / Nasi tuliopata imani kwa mahubiri yao /tunakukiri Wewe kuwa Bwana Mungu wetu / mwingi wa huruma/ mwenye fadhili / si mwepesi wa hasira / mwingi wa rehema na kweli. / (Ayubu 4:3).

Basi, tunaposherehekea Jubilei ya miaka 150 ya Kanisa Katoliki Tanzania Bara / tunakuabudu katika maongozi yako./ Tunakushukuru kwa kuongezeka kwa imani/ inayoonekana katika idadi ya Waamini Walei / Makatekista / Watawa / Mapadri na Maaskofu wazalendo. / Tunakushukuru kwa kutuwezesha kuhudumia taifa letu katika elimu / afya na huduma nyingine za kijamii.

Tunajua kuwa bila wewe hatuwezi kitu / tunakuomba uwe pamoja nasi katika kukabiliana na changamoto mbalimbali kwenye taifa letu siku hizi hasa / ulevi wa pombe na dawa za kulevya / usafirishaji haramu wa binadamu / ugaidi / maradhi, / ubakaji / ulawiti / dhuluma / ushirikina na ulegevu wa dini. / Tunamwomba Mama Bikira Maria /Nyota ya uinjilishaji mpya / na Mlinzi wa Taifa letu /atuombee kwako daima/ ili tuendelee kuihubiri injili yako katika maisha yetu ya kila siku.  Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu.Amina.

Imeidhinishwa kutumika : Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa.

RAIS WA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA.








All the contents on this site are copyrighted ©.