2017-02-17 12:20:00

Barua 1500 zimekusanywa kutoa ushuhuda wa mtawa Lucia wa Fatima


Katika maadhimisho ya miaka 100 ya kutokea kwa mama Bikira Maria wa Fatima, viongozi Katoliki wa Ureno walitangaza Jumatatu 13 Februari 2017 ya kwamba ni maelfu  ya kurasa za barua zilizokusanywa kushuhudia utakatifu wa mtawa Lucia mmoja wa watoto watatu walio shuhudia kutokewa kwa Mama Maria.
Habari kutoka katika Shirika la Habari Katoliki (CAN) linasema, Nyaraka zilizo kusanywa kwa ajili ya Sr Lucia ni barua zaidi ya 15,000 za ushuhuda na barua  nyingine zaidi ambazo zina unga mkono katika utetezi wa kutangazwa mwenye heri. Askofu Virgilio Antunes wa Coimbra Ureno, anabainisha kuwa kurasa zilizokusanywa kwa miaka minne zinauhusu barua binafsi na ushuhuda wa watu zaidi ya 60.


Kurasa hizi zilizo wakilishwa wakati wa maadhimisho ya mtawa Lucia huko Coimbra Askofu anasema pia zitatumwa Vatican kwenye Baraza la mchakato wa kutangaza wenye heri na watakatifu kwaajili ya kupitishwa na baadaye kuendelaa na mchakato wa kuelekea hatua ya pili ya kutangazwa Mtakatifu, lakini kwanza inabidi kupitiwa na kukubaliwa na Baba Mtakatifu Francisko.
Historia ya Bikira Maria wa Fatima ni moja ya historia  maarufu zaidi kwani ilikuwa  tarehe 13 Mei 1917, watoto Francis na Jacinta Marto wenye umri wa miaka 9 na 7 wakiwa na binamu yao mwenye umri wa miaka 10 Lucia Dos Santos walikuwa wakichunga Kondoo kondeni katika mji wa Fatima nchini Ureno ,wakaona kivuli cha mwanamke aliyekuwa amevaa nguo nyeupe na kashika Rosari mikononi mwake.


Baada ya tokeo  la kwanza Bikira Maria aliwatokea tena tarehe 13 ya kila mwezi kuanzia Mei hadi Oktoba.Ujumbe wa Fatima unaweza kuwekwa katika muhtasari hasa  kama wito wa toba , malipizi na maombi.Mwaka 1930 Kanisa lilitangaza tabia zisizo za kawaida za kutokea na ndipo  Madhabuhu ya Fatima ikachaguliwa . Madhabahu hiyo imetembelewa na Papa Paulo wa VI tarehe 13 Mei 1967 na baadaye wakafuata Mtakatifu Yohane Paulo wa II na Baba Mtakatifu Mstaafu Benedikto wa XVI.
Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili amekuwa na ibada pekee maalumu  ya nguvu ya Mama yetu wa Fatima.Baada ya jaribio la kutaka kuwawa mwaka 1981, inasadikika kuishi kwake ni kutokana na muujiza. Kama ishara ya shukrani yeye mwenyewe aliweka risasi iliyo mjeruhi katika taji la Mama wa Fatima.Akiwa katika tukio hilo Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili  alitoa sala yake akasema,” Omba kwa ajili ya ndugu ambaye alitaka kuniua kwa risasi hii, na ambaye kwa moyo wa dhati nina msamehe, kwa kuungana na Kristo na kuhani aliyetoa sadaka,nami natoa mateso yangu kwa ajili ya Kanisa na Ulimwengu”.


Halikadhalika Baba Mtakatifu Francisko anatazamia kutembelea Fatima tarehe 12-13 Mei 2017 kama sehemu ya maadhimisho ya Jubilei ya Karne Moja, tangu Bikira Maria wa Fatima alipowatokea watoto watatu wa Fatima, yaani Francis,Yacinta Marto na Lucia Dos Santos wakiwa wanachunga kondeni. Ikumbukwe kwamba Francis na Jacinta Marto walikufa wakiwa vijana na kutangazwa wenye Heri mwaka 2000. Na mtawa Lucia  Dos Santos amekufa mwaka 2005 akiwa na umri wa miaka 97 katika konventi ya kitawa huko Coimbra.

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.