2017-02-14 15:57:00

Sherehe za maadhimisho ya mashahidi wa Uganda kupamba moto


Tarehe 30 Januari Katibu Mkuu wa Baraza la maaskofu wa Uganda aliitisha washiriki 30  kutoka Jimbo la Hoima, na washiriki hao walitoka katika Kamati 9 za maandalizi ya Sikukuu ya Mshahidi wa Uganda, itakayofikia kilele chake tarehe 3 Juni 2017. Mkutano huo ulihutubiwa na Askofu Vincent Kirabu wa Jimbo la  Hoima.Pamoja na maandalizi yanayo fanyika taarifa inasema kwamba  ni zaidi ya wanakwaya  4000 wameanza maandalizi ya nyimbo kwaajili ya sherehe ya tarehe 3 Juni . Wanakwaya hao wamechaguliwa kutoka kila Parokia za vikarieti 3 za majimbo ambazo ni Jimbo la Hoima Kabale na Masindi.


Hayo ni maadhimisho ya kumbukumbu ya mashahidi , 45 wote wakiwa na Wakatoliki na Waanglikani walio chomwa moto kwa agizo la  mfalme Kabaka Mwanga II na baadaya Mfalme wa Buganda kati ya mwaka 1885 na 1887 wakitetea Imani yao kwa Mungu. Mashahidi 20 walitangazwa wenye heri  tarehe 6 Juni 1920 na Baba Mtakatifu Benedikto wa XV na tarehe 18 Oktoba 1964,Baba Mtaktifu Paul VI akawatangaza kuwa watakatifu, wawili kati yao ni Mtakatifu Andrea Kaggwa na Mtakatifu Anatoli Kiriggwajjo wakiwa wote wawili kutoka katika la Jimbo la Hoima.
Maadhimisho kwa kawaida hukusanya mamilioni ya mahujaji kutoka pande zote za dunia  mara ya mwisho  kuadhimisha sikukuu ya mashahidi katika Jimbo la Hoima ilikuwa mwaka 2001.Hali kadhalika Jimbo la Hoima limekubali kuandaa maadhimisho ya Sikukuu ya mashahidi terehe 3 Juni 2017 katika madhabahu ya Namungongo .


Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya sherehe za mashahidi wa Uganda  kwa mwaka 2017 tarehe 3 Juni katika madhabahu ya Namugongo ametoa taarifa ya kwamba Takribani ya dola za 41,806 zenye thamani ya shilingi milioni 150 za Uganda zimesha tolewa kutoka katika maparokia na makampuni mbalimbali. Anatoa pongezi kwa mchango huo akiwa na matumaini makubwa kufikia malengo ifikapo mwezi Aprili mwaka huu . Hata hiyo kadirio la sherehe zinatakiwa zifikie takribani dola za kimarekani 13,353. Na hivyo  anasema kwamba majimbo yanategemea kuanzisha njia nyingine katika kuhamasisha michango hiyo ili kufikia lengo.

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.