2017-02-04 15:43:00

Kuhudumia masikini ni kazi lakini ni kuwapa matumaini endelevu


Kuhudumia masikini ni kazi lakini ni matumaini, ni maneno ya Sista Emiliana Saptaningsih wa Shirika la mioyo mitakatifu ya Yesu na Maria anayetoa huduma kwenye  utume wa  maeneo duni huko Ufilippine ,lakini ni maeneo yasiyo takiwa kuishi mtu. 
Watu walianza kushi mitaa ya maeneo hayo tangu mwaka 1980 kando kidogo ya Mji Mkuu Manila , sehemu hiyo kwa sasa inajulikana “Bagong Silang.Taratibu mtaa huo ulipanuka na kujaa watu masikini watokao katika mji Mkuu Manila ili kupata mahali pa kijihifadhi.


Tangu kuanza kwa kwake, Bagong Silang imekuwa na watu wengi  zaidi ya 300,000 wanaoishi Katika jitihada za kudhibiti hali hiyo wakuu wa vitongoji walijitahidi kuwapatia familia nyingi eneo kuanzia mita za mraba  50-60 ili wapate kujenga nyumba zao . Hata hivyo miundo mbinu ya ndani ilikuwa siyo ya kutosha kuwasaidia wakazi kutokana na wingi wao na pia ukosefu wa huduma msingi muhimu. 
Katika hali hii ndipo ikaanzishwa kituo cha Mtakatifu Damian, kilichoanzishwa na Shirika la Mioyo Mitakatifu ya Yesu na Maria mwaka 2012 .Watawa na watu wa kujitolea wanashiriki kikamilifu katika huduma ya waoto wenye utapiamlo na mama wajawazito  kwa misaada kwa njia ya miradi. Hali kadhalika wanayo  mipango mingine kwa lengo la wakazi wanaoishi maeneo hayo ikiwa ni elimu,kwa kutoa mafuzo  ya ufundi mbalimbali na upatikanaji wa wafadhili kwaajili ya watoto wapate kusoma  shule.


Juhudi za mipango hii ni kujaribu kutoa matumani kwa watu , sista Emiliana anasema kuwa watu hawa anapaswa wakidhi haja ya mahitaji yao kwa uwepo wa  vifaa mbalimbalimbali, lakini pia ni muhimu kuangalia mahitaji yao kiroho.Anaongeza masikini wa Bagong Silang wana moyo mkuu ambao unazidi kuboreshwa kwa matumaini katika maisha yao  endelevu. “utume wetu ni kuwasaidia waboreshe maisha yao na pia waweze kutambua uwezo wao walio nao na kuwasindikiza kiroho”. Anamalizia kwa kubainisha kuwa jumuiya katoliki inafanya juhudi za pamoja ili kwafikia , kuwasindikiza na kuwatibu masikini wa maeneo hayo duni.

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.