2017-01-18 15:24:00

Asilimia 80% ya wakazi wa Ethiopia hutegemea kulimo na ufugaji


Wakati kaskazini na magharibi ya Ethiopia wana vumilia  uzito  mkubwa wa El Niño, kipeo kipya cha ukame kimejitokeza katika maeneo ya wafugaji wa kusini na kusini-mashariki, kati ya mikoa ya Oromia, kusini mwa Somalia , ambapo mvua ni haba, imechelewa kaida yake , na kusababisha uwepo wa malisho madogo na upatikanaji wa maji. Asilimia 80% ya waethiopia wanategema kilimo na mifugo kuinua kipato chao.Hali hiyo pia imeathiri hata nchi jirani za Somalia na Kenya.Na athari zaidi za ukosefu wa mvua, zitasababisha malisho madogo kwaajili ya mifugo katika miezi ya kwanza ya 2017, na kufanya  kama kawaida yao  kuhama kutokana na ukosefu wa chakula  au vifo vya wanyama wao.


FAO imeomba msaada wa haraka kwaajili ya wachungaji wa Kaskazini ambao wanateseka na ukosefu wa mvua baada ya mafuriko ya El Nino.Hizo ni taarifa kutoka Shirika la Chakula Duniani FAO; wanasema kwamba misaada ya kibinadamu imetolewa kuwasaidia  karibia miaka 50 hivi lakini ukosefu wa mvua wakati wa msimu wa kupanda na pia mvua za El Nino zimendelea kusababisha jumuiya ya wafugaji kuwa na shida kubwa ya maji katika mikoa ya Kusini.


Kwa kujibu suala hili inabidi kusaidia familia ambazo zimeathirika kwani walipoteza kila kitu, au kuuza wanyama na mali zao au wengine kukopa na kurundika madeni.Pamoja na hayo taarifa inaonesha kwamba kutokana na misaada iliyotolewa imepunguza  idadi ya watu watakao hitaji msaada  wa chakula kwa mwaka 2017, kufikia milioni 5,6 pungufu hiyo ni mara  mbili ya takwimu ya mwaka jana 2016 ya  mwezi  8 iliyokuwa imetangazwa na  Shirika la   misaada ya kibinadamu kwa upande wa nchi ya  Ethiopia.


Hati ya Shirika la misaada ya kibinadamu iliyopitishwa hivi karibuni, imeandaliwa kwa mapana kwa pamoja na Serikali ya Ethiopia wakishirikiana pamoja na mashirika ya Umoja wa Mataifa ,yasiyo ya kiserikali na wadau wengine wa maendeleo. Hati hiyo inatazama mada mbalimbali ikiwa ni pamoja na elimu upatikanaji wa maji na lishe.Na inaonesha kwamba ni sekta ya kilimo inahitaji msaada kwa upande wa wachungaji katika maeneo ya wakulima na wafugaji. Jumla ya dola za kimarekani milioni 42 inayotakiwa na kwa sekta ya kuweza kufikia familia milioni 1.9 hasa katika mikoa yenye wafugaji huko kusini na kusini mashariki mwa Ethiopia  kwaajili ya ukame.

 

Na Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.