2016-02-09 15:25:00

Papa: Waungamishaji msichoke kutoa msamaha wa Mungu kwa mdhambi


Mapema Jumanne hii, Baba Mtakatifu Francisko aliongoza Ibada ya Misa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican,  iliyoandaliwa kwa ajili ya Jumuiya ya  Wafranciskani  ” Ndugu Wadogo wa Mtakatifu Francisko”( Wakapuchini) , waliokusanyika  Roma kutoka sehemu mbalimbali za dunia . Mkusanyiko uliolenga kutafakari kwa pamoja  uhusiano  na uwepo wa masalia ya Watakatifu Wawili wenzao,  katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro,  Mtakatifu Pius wa Pietrocina na Mtakatifu Leopoldo wa Mandic,  Wakapuchini , walioyakana maisha ya kidunia na kujiweka katika imani ya kumtumikia Kristo, kama Mapadre.

Baba Mtakatifu katika homilia yake,  aliwaambia  Wakapuchini hao kwamba, , anazungumza nao kama mmoja wao  katika udugu wa Wakapuchini, na kupitia kwao alipenda kufikisha ujumbe wake kwa waungamishaji wote , hasa katika mwaka huu wa huruma ya Mungu , kwamba, maungamo ni kwa ajili ya kutoa msamaha kwa mwenye  dhambi anayeugamana. Na hivyo muungamishaji anapaswa  kutoa msamaha,  na si kumpiga mjeledi wa malipizi muungamaji .

Aliongeza kuwaasa, mtu anayekuja kuungama, ni mtualiyepondeka moyo kw amakosa aliyoyafanya na hivyo  anakuja tafuta faraja , kuomba msamaha, ili nafsi yake ipate kuwa na  amani. Kwa hiyo, anategemea kumkuta baba aliyetayari kumkumbatia na kumwambia Mungu anakupenda. Muungamaji atapenda kumkuta Padre  anayemfanya ajisikie vizuri, kujenga upya mahusiano yake yakuwa karibu na Mungu.  Papa alieleza na kuonyesha  kutambua kwamba,  wengi wao wamesikia watu wakisema, kwa padre yule kwamwe siwezi kwenda kuungama, kwa kuwa siku moja alinifehehesha kwa maswali mengi yake, Padre yule alinifanyia hiki au kile na sasa siwezi kwenda kwake… 

Baba Mtakatifu alieleza na kuwataka  wote waliopewa dhamana hii ya kuwa  waungamishaji na watoaji wa msamaha kwa  jina la Kristo,  kutopoteza thamani ya dhamana hii iliyotolewa bure kwao kama zawadi maalum toka kwa Bwana katika kusamehe. Na hivyo aliwaomba wasichoke kusamehe.

Aidha Papa alionyesha  hamu yake, katika kuwaona  waumngamishaji kila mahali wakiwa na mawazo mapana na  nyoyo wazi ,wasiochoka kamwe   kuwa vyombo vya kutoa Msamaha wa Mungu na wenye kuelewa mateso ya dhambi , kwa sababu wao pia  lazima kutambua kwamba ni  wenye dhambi , wanaohitaji  kwanza kupata  huruma ya Mungu ya kuokoa. Amewataka wote, waombe kutoka kwa  Bwana neema ya kuwa mfano wa huruma ya Mungu  na si kuwa mtu Mkatili. Wanapaswa  kuonyesha sura ya kuwa wasamehevu,  wapatanishi na watu wa amani.   

Baba  Mtakatifu alieleza na kukumbusha kuwa,  kuna lugha  nyingi katika maisha , lugha ya kuzumgumza maneno na pia kuna lugha ya vitendo.  Na kwamba msamaha ni mbegu ya  upendo  na huruma ya  Mungu . Amewaataka   kama waungamishaji katika nafasi  ya Yesu , aliyetoa maisha yake yote katika sala kwa muda mrefu, na pia  kama walivyokuwa wenzao  Mtakatifu Pio wa Pietrolcina na Mtakatifu Leopoldo , walivyotumia muda wao mwingi wakiungamisha watu  nao pia wafanye kazi hiyo , kwa moyo wote , kumfukuza shetani katika mioyo ya watu. 








All the contents on this site are copyrighted ©.