2015-08-15 12:16:00

Kardinali Parolin azungumzia umuhimu wa muungano wa imani na utamaduni


(Vatican Radio) Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Nchi ya Vatican,  Ijumaa (14 Agosti) alisisitiza umuhimu wa kuwepo muungano thabiti kati ya imani na utamaduni mahalia. Kardinali alieleza hilo akiwa katika ziara  aliyoianza tarehe 10 Agosti kwanza kwa kutembelea Indonesia na baadaye kwenda Timor ya Mashariki ambako amekuwa kwa muda wa siku tatu kwa ajili ya kilele cha maadhimisho ya kitaifa tarehe 15 Agosti, kwa ajili ya kutimia karne tangu uinjlishaji uanze katika taifa hilo. .

Ijumaa 14 Agosti ,wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa kwa heshima yake na Waziri Mkuu Rui Maria de Araujo wa Timor ya Mashariki, Kardinali Parolin, akiongea kama mwakilishi wa Papa katika maadhimisho ya kutimia karne tano ya Uinjilishaji  Timor-Mashariki na utiaji wa  saini katika Mkataba kati ya Jimbo la Papa na Timorya Mashariki , alitoa shukurani zake za dhati kwa makaribisho mazuri aliyoyapata akiwa katika nchi hii ya Timor ya Mashariki.

Aliongeza “ ni heshima kubwa kuwa mahali   hapa na hasa kama mwalikishi wa Baba Mtakatifu Francisko, ambaye daima hupenda kukumbusha watu wote,  umuhimu wa kuzingatia uadilifu iwapo, kwa ajili ya kuwa na dunia yenye maisha ya watu yaliyojengwa katika msingi wa  haki , mshikamano na udugu".  Na akasema , "Siyo siri, uhusiano ya  Jimbo Takatifu na Timor ya Mashariki  una mambo mengi ya kawaida ambamo wanashirikiana kimaadili,  kwa ajili ya kuhakikishia maendeleo muhimu endelevu kwa watu wa Timor. Uhusiano uliosimikwa katika mzizi wa  muungano wa kipekee wa imani na utamaduni wa miaka mingi ambao mwaka huu kihalali wanasherehekea kupita kwa miaka mia tano tangu kuanzishwa katika taifa hilo”.

Kardinali Parolin aliendelea kueleza kwamba, ni wazi hawawezi kukanusha ukweli kwamba muungano huu unaweza tu kuwa endelevu iwapo kila upande utaendelea kudhamiria kuheshimu majukumu yaliyotajwa katika mkataba juu ya utendaji wa ndani ya serikali, na ndani ya asasi za kiraia, na  ndani ya Kanisa kama wachungaji wa kundi walilopewa.  Na akataja kwamba, historia imeonyesha kwa bahati mbaya, wakati umoja kama huu, unapopuuzwa au kuchukuliwa kama jambo jepesi,  hujengwa mwelekeo wa kuepuka misingi ya maadili ya imani na utamaduni. Na hivyo mara husababisha kuporomoka kwa haki za msingi za binadamu, zikipuuzwa na hata kukataliwa.

Katika hali hiyo, Kardinali alisisitiza ni muhimu kwa  Mamlaka zote mbili serikali na Kanisa, kufanya kazi pamoja kwa  kuheshimiana na uelewa kwamba wote utumishi wao ni kwa manufaa ya  watu wote,  katika hamu yao kwa kutambua maadili yao na matarajio yao . Na hivyo katika sherehe hizi za kutimia karne tangu Habari njema ya wokovu wa Kristo kufikishwa Timor ya Mashariki, linakuwa ni tukio muhimu linaloonyesha muungano thabiti wa imani na utamaduni katika taifa hilo pendwa la Timor ya Mashariki.  Na hiyo ndiyo maana katika maadhimisho ya Jubilee hii ya karne Tano za uinjlishaji pia  imekuwa ni nafasi nzuri ya kuthibitisha kwa mara nyingine uwepo wa ushirikiano kati ya kanisa Katoliki na serikali, kwa kuweka saini katika Mkataba huu wenye  viungo vya kihistoria, ikilenga kuwahakikishia wote  kwamba  muungano huu si tu unaendelea hivihivi lakini kwa uwepo wa hoja ya nguvu ya ushirikiano na mshikamano kwa manufaa ya watu wote wa Timor wenyewe.

Aidha alitaja kwamba kitendo cha kusaini Mkataba imekuwa ishara kubwa ya kuonekana katika njia zote za  mawasiliano kwa ya manufaa ya jamii na Kanisa. Ni ishara kubwa inayoonyesha matunda mazuri yalizozaliwa kutokana na mahusiano mazuri kati  Kanisa na Serikali. Na ni hatua muhimu katika hija ya  Kanisa Katoliki kwa  watu wa Timor ya Mashariki, walioifanya pamoja kwa miaka mia tano iliyopita. Uhusiano huu ni wa kipekee, na wenye thamani kubwa kwa Jimbo Takatifu na Timor ya Mashariki, ushirikiano ulio wazi hata katika Katiba ya Timor ya Mashariki.

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.